Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii

UPANDE wa mashtaka katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kuwa inatarajia kuleta mashahidi 15 na vielelezo vitatu katika kesi hiyo. 
Wakili wa Serikali, Wankyo Saimon akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga wameeleza hayo leo Desemba 13, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi Mara baada ya kumaliza kumsomea Zitto maelezo ya awali ( PH).
Katuga amedai watakuwa na mashahidi 15 na vielelezo viwili vya kimaandishi na kielelezo kimoja cha kieletroniki.Ameongeza kudai kuwa jinsi kesi itakavyoendelea kusikilizwa wanaweza kuongeza mashahidi na vielelezo au kupunguza mashidi, kwa sababu hata baada ya Zitto kusomewa maelezo hayo Leo na kuyajibu wanaweza kuwapunguza.
Kutokana na maelezo hayo, Hakimu Shaidi alimpa nafasi Wakili wa Zitto, Peter Kibatala kuzungumza, ambapo alidai kuwa wataongea baada ya 
upande wa mashtaka kufungua ushahidi wao.Pia Katuga aliiomba Mahakama iwape muda wa wao kuweza kutoa nakala ya mtoa taarifa ili waweze na kuwapatia upande wa utetezi kama sheria inavyoelekeza.

Awali, Wakili Wankyo akimsomea Zitto PH amedai Oktoba 28, 2018 mshtakiwa akiwa katika mkutano na waandishi wa habari, uliyofanyika katika Makao Mkuu ya ofisi ya Chama cha ACT_Wazalendo alitoa maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...