Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Mfuko wa Jimbo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kupitisha miradi itakayosaidiwa na Mfuko huo, Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini Edward Mwalongo amesema kuwa kiasi cha shilingi milioni 40 kitatumika kununulia vifaa vya ujenzi kulingana na mahitaji ya mradi husika na vitagawiwa kwenye Kata 13 za jimbo hilo ili kuweza kuchochea na kuchangia kasi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mwalongo amesema kuwa vipaumbele vya Mfuko wa Jimbo ni kusaidia miradi ya afya, elimu pamoja na utawala mara baada ya kufanyika upembuzi yakinifu na kubaini mahitaji ya vifaa kwenye miradi iliyoibuliwa na wananchi na ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019 mfuko wa jimbo umefanikiwa kufanya jambo la upekee katika sekta ya elimu tofauti na vipindi vingine jambo ambalo limepokelewa kwa furaha na wanafunzi na uongozi wa Ruhuji shule ya Msingi.

“Kitu cha pekee ambacho Mfuko wa Jimbo umefanya katika mwaka huu wa fedha 2018/2019 ni kusaidia ujenzi wa jiko maalumu katika Shule ya Msingi Ruhuji ambalo litakua linatumia kuni kidogo, na rafiki wa Mazingira lakini pia ununuzi wa sufuria aina ya “Stainless steel”ambayo ni imara na haipati kutu na itatumika kwa muda mrefu. Hii itaonesha njia kwa Shule nyingine za Msingi na Sekondari katika Jimbo la Njombe kwamba jiko bora na sufuria bora liko Ruhuji Shule ya Msingi na wanaweza kufika pale kujifunza.”Alisema Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini Mhe. Mwalongo.
Mbunge wa Njombe mjini Edward Mwalongo(wa kwanza kulia) akikagua ujenzi wa miradi mbalimbali wakati wa ziara ya Kamati ya Mfuko wa Jimbo iliyofanywa kwa lengo la kukagua na kupitisha miradi jimboni kwake.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...