Zawadi ya wiki ya shilingi milioni kumi inayotolewa katika kampeni inayoendelea ya Tigo Jigiftishe, ilikabidhiwa mwishoni mwa wiki kwa Flora Somba ambaye ni mkazi mjini Morogoro . 

Flora anakuwa ni mshindi wa nne kupata zawadi ya shilingi milioni kumi baada ya David Mmuni, Iyaka Muinga wote wa Dar es Salaama pamoja na Mbwana Mbela mkazi wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma. Akiongea huku akibubujikwa na machozi wakati akikabidhiwa zawadi yake, Flora ambaye anafanya kazi za vibarua kwenye ujenzi kama kubeba zege, alisema Mungu amemtendea miujiza kupitia Tigo Jigiftishe. 

“Nalea watoto wawili peke yangu, mimi ndiyo baba na mimi ndiyo mama. Binti yangu Irene alilazimika kuacha shule kwa sababu sikiuweza kumlipia ada, nashukuru Mungu sasa ataweza kurudi shuleni,asante Tigo kwa kubadilisha naisha yangu” alisema .Flora alisema fedha atakazopata pamoja na kusaidia ada za watoto, atajitahidi kujenga nyumba walau ya vyumba viwili ili kuachana na nyumba za kupanga na kuongeza kuwa fedha itakayobaki atafungua biashara itakayomsaidia kuhudumia familia yake. 

Hafla ya kukabidhi mshindi wa milioni 10 zawadi yake, ilienda sambamba na kuwakabidhi washindi wengine saba wa shilling milioni moja moja kutoka mkoa wa Morogoro zawadi zao .Akiongea wakaati wa hafla hiyo, Mkurugenzi wa Tigo kwa Kanda ya Pwani Joseph Mutalemwa alisema promosheni ya Jigiftishe inalenga kuwazawadia wateja wanaotumia huduma za mtandao huo katika kipindi hiki cha sikukuu. 
 Mshindi wa zawadi ya shilingi milioni 10 ya Tigo Jigiftishe Flora Somba  kutoka Morogoro (wa kwanza kushoto) akiwa na uso wa furaha na binti yake Irene Hatibu (wa pili kushoto) muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi yake.  Wa kwanza kulia ni mtangazaji wa Clouds FM Mina Ally akifuatiwa na Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Pwani Joseph Mutalemwa. Wengine ni Viongozi wa Tigo Kanda ya Pwani.

 Mshindi wa zawadi ya shilingi milioni 10 ya Tigo Jigiftishe Flora Somba  kutoka Morogoro akijifuta machozi  ya furaha muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi yake mjini Morogoro mwishoni mwa wiki. Kulia ni mtangazaji wa Radio Clouds FM Mina Ally na wengine ni viongozi wa Tigo kanda ya Pwani.

 Mshindi wa zawadi ya shilingi milioni 10 ya Tigo Jigiftishe Flora Somba  kutoka Morogoro (wa tatu kulia), akiwa na washindi wa shilingi milioni moja moja kutoka mkoani Morogoro muda mfupi baada ya wote kukabidhiwa zawadi zao. Kulia ni mtangazaji wa Clouds FM Mina Ally na wengine ni viongozi wa Tigo Kanda ya Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...