Kitita cha shilingi milioni 10 cha mshindi wa kila wiki katika promosheni inayoendelea ya Tigo Jigiftishe, kimenyakuliwa na Iyaka Seifu Muinga, anayefanya kazi ya kuosha magari Tabata jijini Dar es Salaam.
Muinga anakuwa ni mshindi wa pili wa zawadi ya shilingi milioni 10 baada ya milioni kumi ya kwanza kuchukuliwa na David John Mmuni mkazi wa Changanyikeni jijini Dar es Salaam.

Akipokea zawadi yake katika eneo analofanyia  kazi kutoka kwa Meneja wa Biashara wa Tigo, Suleiman Bushangama, mshindi huyo alielezea furaha yake na ksema kuwa Tigo imemkomboa kwa kuwa amepata mtaj wa kufungua biashara.

‘Nimefurahi sana kuibuka na mtaji huu kutoka promosheni ya Jigiftishe. Nitatumia pesa hizi kufungua biashara, ila kusema kweli sina mpango wa kuacha kazi yangu ya sasa,” Iyaka alisema huku akishangiliwa na wafanyakazi wenzake waliomsindikiza jukwaani kupokea zawadi.

Akiongea  wakati akimkabidhi mshindi huyo zawadi yahe, Bushangama aliwataka wateja kuendelea kutumia huduma mbali mbali za Tigo ili kujishindia mamilioni ya shilingi yaliyotengwa kwa ajili ya kuwazawadia katika msimu huu wa sikukuu.
 
 Mmoja wa washindi wa zawadi ya kilaa siku ya shilingi milioni moja kwenye promosheni ya Jigiftishe inayoendeshwa na kampuni ya Tigo, Asha Shaban (wa pil kulia) akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Meneja Bidhaa waa Tigo, Suleiman Bushangama (kushoto) pamoja na Jafary Othman – Mtaalam wa Huduma za Tigo (wa pili kushoto) katika hafla fupi ya kuwakabidhi washindi zawadi zao iliyofanyika eneo la Tabata jijini Dar es Salaam. Wa kwanza  kulia ni Balozi wa promosheni hiyo, mtangazaji Mina Ally.    
6J9A0772-min
Mmoja wa washindi wa zawadi kila siku ya shilingi milioni moja kwenye promosheni ya Jigiftishe inayoendeshwa na kampuni ya Tigo, Anna Eliudi Makala  (wa pili kulia) akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Meneja Bidhaa wa Tigo, Suleiman Bushangama (kulia) pamoja na Jafary Othman – Mtaalam wa Huduma za Tigo (wa pili kulia) katika hafla fupi ya kuwakabidhi washindi zawadi iliyofanyika Tabata jijini Dar es Salaam. 
6J9A0782-min
Mshindi wa zawadi ya wiki ya shilingi milioni 10 katika promosheni ya Jigiftishe inayoendeshwa na kampuni ya Tigo, Iyaka Seifu Muinga (kulia) akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Meneja Bidhaa wa Tigo, Suleiman Bushangama (kulia) pamoja na Jafary Othman – Mtaalam wa Huduma za Tigo (wa pili kulia) katika hafla fupi ya kumkabidhi washindi zawadi eneo la Tabata jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Balozi wa promosheni hiyo, mtangazaji Mina Ally.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...