Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

KAMATI ya Ulinzi na Usalama ikongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo imeamua kufanya operesheni maalumu ya kusaka na kuwaondoa watu waliovamia maeneo ya hifadhi ya Mbarang'andu ambapo kuna watu kadhaa wamekamatwa na sasa wanaohojiwa.

Akizungumzia operesheni hiyo Mkuu wa Wilaya Kizigo ameiambia leo, Michuzi Blog kuwa wameanza kuifanya juzi na jana (Desemba 4 na Desemba 5 mwaka 2018) ambapo mbali ya kamati ya ulinzi na usalama pia kulikuwepo na vikosi kazi na timu ya wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri ya wilaya hiyo na kwamba uamuzi huo wa kufanya msako umekuja baada ya doria ya kwanza iliyofanyika kwa njia ya anga (ndege) ambapo walijionea uharibifu uliofanyika kwenye hifadhi ya Ushoroba wa Selous , Niassa, Mbarang'andu , Kisungule na Kimbanda.

"Kwa kutumia usafiri wa anga ambao tumefanya kwenye maeneo mbalimbali ya hifadhi tumejionea namna ambavyo kuna uharibu wa mazingira.Hivyo jana tumeamua kufanya msako maalumu wenye lengo la kuwaondoa wavamizi ambao wanaharibu hifadhi hiyo,"amesema Mkuu wa Wilaya Kizigo.

Amesema katika kuhakikisha wanafanikiwa kwenye operesheni hiyo juzi na jana waliamua kwenda kwa miguu maeneo ambayo yamefanyiwa uharibifu na tayari kuna baadhi ya watu ambao wamewakamata kwa kutuhuma za kuharibu hifadhi ambapo pia amesema wapo watu ambao wanaingia kwenye msitu huo kwa ajili ya kufanya ujangiri kwa kuua wanyama.


KAMATI ya Ulinzi na Usalama ikongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo wakiendelea kukamata vifaa mbambali vya watu waliovamia maeneo ya hifadhi ya Mbarang'andu ambapo kuna watu kadhaa wamekamatwa na sasa wanaohojiwa.
Sehemu ya Kamati i ya Ulinzi na Usalama ikongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo (wa pilia kulia) wakiwa kwenye operesheni maalumu ya kusaka na kuwaondoa watu waliovamia maeneo ya hifadhi ya Mbarang'andu ambapo kuna watu kadhaa wamekamatwa na sasa wanaohojiwa.
Baadhi ya Watuhumiwa waliokamatwa na kamati ya Ulinzi na Usalama ikongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo  (hayupo pichani) walipokuwa wakifanya operesheni maalumu ya kusaka na kuwaondoa watu waliovamia maeneo ya hifadhi ya Mbarang'andu ambapo watu kadhaa wamekamatwa na sasa wanaohojiwa.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...