Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii 

Mchezaji Mohamed Issa 'Banka' ameruhusiwa kuanza mazoezi wakati akikaribia mwisho wa adhabu yake ya kufungiwa baada ya kubainika kutumia dawa zisizoruhusiwa michezoni aina ya bangi. 

Banka baada kubainika kutumia dawa hizo alifungiwa kwa kipindi cha miezi 14 kuanzia Disemba 9,2017 na adhabu kumalizika Februari 8,2019. 

Pamoja na kuruhusiwa kuanza mazoezi Banka kucheza mchezo wowote ule zaidi ya kufanya mazoezi. Mchezaji huyo alifungiwa na Kamati ya kuzuia na kupambana na dawa zisizoruhusiwa michezoni ya Kanda ya Tano Africa (RADO). 

Banka alisajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili katika dirisha la usajili la mwezi June akitokea timu ya Mtibwa Sugar lakini hakuweza kushiriki kwenye mchezo wowote kutokana na kufungiwa kutokushiriki masuala ya kimichezo ikiwemo kufanya mazoezi sehemu atakayoonekana na watu.Adhabu yake inatarajiwa kumalizika mwezi Februari mwakani na matarajio yake ni kujiunga na timu yake mpya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...