Na Chalila Chibuda, Blogu ya Jamii
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunatus Muslim amewataka madereva wa kufuata sheria za Usalama ili kuokoa maisha ya wasafiri. Muslim aliyasema hayo wakati alipofanya ziara katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam, amesema kuwa katika mwisho wa mwaka kumekuwa na ungezeko la wasafiri nchi nzima hivyo madereva wazembe hawawezi kuvumiliwa hata kwa uzembe wanaoufanya.

Aidha amesema kuwa wataofanya makosa kwa kujirudia watawanyanga leseni na kutakiwa kurudi darasani ili wakajifunze udereva. "Kazi ya Udereva lazima iheshimike kwa kila mmoja awafuate sheria zilizoekwa na ziko wazi katika kufanya abiria kuwa salama katika safari wanazozifanya"amesema Muslim.

Hata hivyo amesema ukaguzi huo katika kituo cha Ubungo ni wa kila hivyo hakuna gari basi bovu litalofanya safari likwa na ubovu. Amesema usafiri kwa abiria ni kuwasafirisha kwa Usalama na sio kuwaua au kusababisha ulemavu wa kudumu.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunatus Muslim akiwa katika kituo cha mabasi Ubungo kwa akiangalia ukaguzi mabasi katika kituo cha mabasi leo jijini Dar es Salaam.
Ukaguzi chini ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunatus Muslim katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
  Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Fortunatus Muslim akiangalia ukaguzi na unaofanywa na Askari wa Kikosi hicho Ibrahim Samwix wakati alipofanya ziara katika kituo cha mabasi ya Ubungo jijini Dar es  Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...