Na Imma Msumba Arumeru

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amefanya ziara ya kustukiza usiku wa manane katika Hospitali mbili za Wilaya na kujionea hali ya utoaji wa huduma za Afya nyakati za Usiku , ziara ambayo alianza saa Saba na nusu Usiku mpaka saa kumi na moja alfajiri.

Hatua ya Mhe Muro kufanya ziara ya kushtukiza nyakati za Usiku katika hospitali imekuja Kutokana na kuwepo Kwa malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi ambao wameonyeshwa kukerwa na huduma duni za Afya zinazotolewa nyakati za Usiku ikiwemo kutokuwepo Kwa wataalamu katika maeneo yao ya kazi kama inavyotakiwa Kwa mujibu wa sheria, Kanuni na taratibu.

Akiwa katika Hospitali ya Halmashauri ya wilaya (ARUSHA DC) Hospitali ya Oltrumet Mhe. Muro Alifika katika Eneo la mapokezi ambalo mbali na milango kuwa wazi pamoja na nyaraka na baadhi ya Madawa na vifaa tiba lakini hapakuwa na mtu yoyote katika eneo hilo na badala yake kazi ya mapokezi aliachiwa Askari mgambo anaelinda hospitali hiyo ambapo huwapokea wagonjwa na kisha kwenda KUWAAMSHA WAHUSIKA AMBAO MUDA MWINGI WANAKUWA Wamelala tukio ambalo limeshuhudiwa na Mhe Muro ambae alilazimika kwenda katika Hospitali hiyo akiwa na Usafiri Binafsi wa pikipiki na gari lingine la kawaida moja.

Pia Dc Muro alitembelea katika jengo la upasuaji na kukuta tukio la kukera ambapo wauguzi na wahusika wa chumba hicho walikuwa wamelala uku wamejifunika mablanketi hatua iliyomlazimu Mhe Muro kuwaamsha jambo ambalo liliwafanya wakimbie wakihisi wamevamiwa na Mzimu.

Pamoja na kuwepo Kwa changamoto hizo, Mhe Jerry Muro alioonyeshwa kufurahishwa na kitendo Cha muuguzi wa zamu katika jengo la kujifungulia kina mama ambae mbali na kuwa mwenyewe lakini alikuwa akitimiza wajibu wake wa kuendelea kuwahudumia kina mama ambao baadhi walikuwa katika hatua za kujifungua.
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro Akizungumza na Waaguzi walikuwa zamu katika hospital ya Halmashauri ya Meru ( Tengeru) baada ya kufanya ziara yake ya kushtukiza usiku wa manane katika hospital hiyo.
 Dc Muro Akizungumza na moja ya wagonjwa walikuwa wamelazwa katika hospital ya Halmashauri ya Arusha Dc ( Oltrument) usiku wa kuamkia leo

 Dc Muro akipakua moja ya Nyaraka za Hospital ya Halmashauri ya Arusha Dc ( Oltrument ) alipozikuta katika chumba cha mapokezi kilichokuwa wazi na hapakuwa na mhudumu kwa muda huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...