Na Zanab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mahafali ya kumi na moja (11) ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yamefanyika jana kwa jumla ya wahitimu 1769 wametunukiwa katika ngazi mbalimbali.

Kwenye mahafali hayo wahitimu 1736 wametunukiwa digrii za awali katkka fani mbalimbali, 26 wakitunukiwa stashada ya uzamili katika elimu na 7 wakitunukiwa shahada ya umahiri.

Akitoa hotuba kwa Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es salaam Dkt Jakaya Mrisho Kikwete , Rasi wa Chuo Kikuu Kishirikishi Professa Bernadeta Killian amesema kuwa kati ya wahitimu wote wa mwaka huu wanaume ni 1255 na wanawake ni 514.

Amesema idadi ya wahitimu kwa upande wa digrii za awali ni kubwa ikilinganishwa na wahitimu wa miaka yote iliyopita, kwani wahitimu wa digrii za awali kwa mwaka 2017 ilikua ni 1443 ambalo ni ongezeko la wahitimu 239 na kufikia 1736 na wahitimu wa masomo ya sayansi kuongezeka mara mbili kutoka 231 kwa mwaka 2017 kufikia 472 kwa mwaka 2018.
Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dkt Jakaya Kikwete akitoa cheti kwa Mwanafunzi Bora wa kike kutoka kitivo cha Elimu Irene Loshiro wakati wa mahafali ya 11 ya Chuo Kikuu Shirikishi cha Elimu Dar es Salaam (DUCE).Mahafali ya kumi na moja (11) ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) yamefanyika jana ambapo jumla ya wahitimu 1769 wametunukiwa katika ngazi mbalimbali.
Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam Dkt Jakaya Kikwete akitoa cheti kwa Mwanafunzi Bora wa kiume kutoka kitivo cha Sayansi Mohamed Hassan wakati wa mahafali ya 11 ya Chuo Kikuu Shirikishi cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) .
Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam Dkt Jakaya Kikwete akiwa na Mwanafunzi Bora wa kike kutoka kitivo cha ElimuIrene Loshiro na Mwanafunzi bora wa Kiume Kitivo cha Sayansi Mohamed Hassan wakati wa mahafali ya 11 ya Chuo Kikuu Shirikishi cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...