Kampuni ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania imeendelea kung’aa kwenye Tuzo za Mwajiri Bora (EYA) za mwaka 2018 baada ya kuibuka mshindi wa tuzo ya ushirikishaji mzuri wa wafanyakazi (the Employee Engagement Company of the Year 2018) kwa mwaka 2018.

Pamoja na tuzo hiyo kampuni hiyo ambayo imekuwa miongoni mwa wadhamini wakubwa na tuzo hizo, pia ilifanikiwa kutwaa tuzo nyingine ya mahusiano mazuri ya kikazi (Industrial relations). Kila mwaka Chama cha Waajili Tanzania (ATE) kimekuwa kikiandaa tuzo maalum kutambua wanachama wake wake ambao wanafanya vizuri katika masuala mazima ya rasilimali watu ikiwemo kuwa sera nzuri katika nyanja hiyo.

"Mafanikio ya Puma katika kutoa huduma nzuri kwa wateja wetu kwa kiasi kikubwa yanachangiwa na jitihada madhubuti zinazofanywa na wafanyakazi wetu ikiwemo kujitoa kwa dhati katika kutimiza majukumu yao," alisema Dominic Dhanah, Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo. 

Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah akitoa neno la shukrani wakati wa Tuzo za Mwajiri Bora (EYA) za mwaka 2018 zilizoandaliwa na Chama cha Waajili Tanzania (ATE) na kufanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Puma Energy ilifanukiwa kuibuka mshindi wa tuzo ya ushirikishaji mzuri wa wafanyakazi (Employee Engagement Company of the Year 2018) kwa mwaka 2018 pamoja na Tuzo ya Mahusiano mazuri ya kikazi (Industrial relations).
Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah (kulia) pamoja na Meneja Rasilimali Watu Kampuni ya Puma Energy Loveness Hoyange wakionyesha tuzo ya ushirikishaji mzuri wa wafanyakazi (Employee Engagement Company of the Year 2018) kwa mwaka 2018 pamoja na Tuzo ya Mahusiano mazuri ya kikazi (Industrial relations) mara baada ya kukabidhiwa tuzo hizo kwa niaba ya kampuni hiyo.
Meneja Mkuu wa Puma Energy Tanzania, Dominic Dhanah (wa tatu kulia waliokaa), Meneja Rasilimali Watu Kampuni ya Puma Energy Loveness Hoyange (kulia kwake) wakifurahia pamoja na wafanyakazi wengine wa kampuni hiyo mara baada ya kukabidhiwa tuzo ya ushirikishaji mzuri wa wafanyakazi (Employee Engagement Company of the Year 2018) kwa mwaka 2018 pamoja na Tuzo ya Mahusiano mazuri ya kikazi (Industrial relations) kwenye wa hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...