Na. VERO IGNATUS, ARUMERU

Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mhe John pombe magufuli anatazamia kuweka jiwe la msingi katika mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Arusha na baadhi ya maneo ya wilaya ya Arumeru

Mradi huo uliotiliwa saini hivi karibuni utazinduliwa katika kijiji cha kimyaki majira ya saa nne asubuhi na baadae kuzungumza na wananchi katika kijiji cha mringarimga

Wakizungumzia hali ya maji mkazi wa eneo mringaringa Josephat Joshua amesema wakinamama wanalazimika kwenda kutafuatamaji ya kunywa kutoka mringaringa kilometa mbili katika sehemu inayoitwa njoro au kwa wavii.Wakati mwingine sisi wakina baba tunabakia na watoto nyumbani.

'' Wakinamama wanafuata maji, hadi arudi nyumbani anakuwa tayari amechoka sana kutokana na kufuta maji umbali wote huo bado majukumu mengine yanamsubiria"alisema Joshua.Kwa akizungumza kwa bi Miriam Zakayo amesema inawalazimu kutembea umbali mrefu na kushindwa kutimiza majukumu yao kwa wakati 

'' Maji tunayoayatumia ni ya mto nayo yanachukua muda mrefu hadi kufunguliwa kwa sababu wengine tunayatumia katika mifugo, mashamba, hivyo tukitaka maji ya kunywa tunayafuata mbali"alisema Miriam.Mkazi mwingine wa kijiji hicho Saning'o Lebang'ute Laizer amesema kwa ujio wa Rais Magufuli kwao ni neema kwani itawatatulia tatizo hilo sugu la maji safi, barabara na umeme

''Tunashukuru sana kwa kuja kutufikia kwetu ni neema, barabara, hii inawahudumia watu wa kimmyaki, Ilikiding' a na Sambasha, mradi wa umeme, ni fursa kwetu pia"alisema Laizer.
 Mkazi wa kijiji cha mringarimga Miriam Zakayo akienda kufuata maji safi umbali wa km mbili kutoka kijiji cha Kimnyaki.Aidha katika kuhakikisha tatizo la upatikanaji  Maji safi na salama wilayani Arumeru linapungua ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Dkt John pombe magufuli leo anatarajia kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika mradi Mkubwa wa uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Arusha na baadhi ya maneo ya wilaya ya Arumeru.
Mkazi wa kijiji cha mringarimga Miriam Zakayo na wananchi wengine wakienda kufuata maji safi umbali wa km mbili kutoka kijiji cha Kimnyaki,katika kuhakikisha tatizo la upatikanaji wa Maji safi na salama wilayani Arumeru,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Dkt John pombe magufuli anatarajia kuzindua na kuweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Arusha na baadhi ya maneo ya wilaya ya Arumeru.
Pichani kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo na Wananchi wa Arumeru akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro kwa pamoja wakimkaribisa Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika ziara rasmi ya kikazi katika wilaya ya Arumeru leo Jumapili katika kata ya Kimnyak na kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa visima vikubwa vya maji zaidi ya 20 ambavyo ni Sehemu ya Mradi mkubwa wa Maji Kwa Jiji la Arusha ambao utasaidia pia kutoa huduma ya Maji katika kata Saba za Wilaya ya Arumeru , Mradi utakuwa na thamani ya zaidi ya Bilioni 500.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...