Na Stella Kalinga, Simiyu
Mkoa wa Simiyu umejipanga kuandaa mwongozo wa uwekezaji  kwa kila Kijiji na Mtaa utakaobainisha fursa za uwekezaji zilizopo katika kijiji na mtaa husika katika vijiji vyote 471 na Mitaa 92 ya wilaya zote tano za Mkoa huu, ikiwa ni maandalizi ya utekelezaji wa Falsafa ya Bidhaa Moja Kijiji Kimoja(OVOP) mwaka 2019/2020.

 Hayo yamebainishwa  Desemba 11, 2018 Mjini Bariadi katika kongamano la kuwajengea uwezo Watendaji wa Vijiji 471, Watendaji wa Mitaa 92, Watendaji wa Kata 130 na Maafisa tarafa 16 juu ya kuibua fursa za uwekezaji kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa, kwa kushirikiana na Wataalam kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF), ambalo pia limewahusisha viongozi na watendaji wa Chama na Serikali ngazi ya wilaya na Mkoa.

Awali akifungua kongamano hilo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mkoa huu unatekeleza Falsafa ya Bidhaa Moja Wilaya ambayo ilianza baada ya ESRF kufanya utafiti na kuibua fursa 26 ndani ya mkoa na sasa inajipanga kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na kuanza utekelezaji wa Bidhaa Moja Kijiji Kimoja.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Watendaji wa Vijiji 471, Watendaji wa Kata 130, Maafisa Tarafa 16 katika kongamano lililolenga kuwajengea uwezo wa namna ya kuibua fursa za uwekezaji kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa, kwa kushirikiana na Wataalam kutoka ESRF, ambalo pia liliwahusisha viongozi na watendaji wa Chama na Serikali ngazi ya wilaya na Mkoa.
  Mtafiti Mkuu Mshiriki kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF), Prof. Samwel Wangwe akiwasilisha mada kwa Watendaji wa Vijiji 471, Watendaji wa Kata 130, Maafisa Tarafa 16 juu ya  namna ya kuibua fursa za uwekezaji kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa mkoani Simiyu, lililofanyika Mjini Bariadi Desemba 11,2018.
Baadhi ya Watendaji wa Vijiji, Mitaa na Kata wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani)  katika kongamano la kuwajengea uwezo Watendaji hao juu ya  namna ya kuibua fursa za uwekezaji kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa, lililofanyika Mjini Bariadi Desemba 11,2018.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wataalam kutoka ESRF, Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakiwemo Watendaji wa Vijiji, mitaa na kata (wenye fulana za rangi ya yachungwa na nyeupe) , baada ya kongamano la kuwajengea uwezo viongozi hao juu ya namna ya kuibua fursa za uwekezaji, kwa ajili ya kuandaa mwongozo wa uwekezaji kwa kila kijiji na mtaa, lililofanyika Mjini Bariadi Desemba 11, 2018.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...