Wananchi wameombwa kutoa taarifa mapema kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa miradi ya maendeleo wanaoitilia shaka kugubikwa na ufisadi ili kuokoa matumizi mabaya ya fedha za umma. Akizungumza wakati wa kongamano la kujadili utatuzi wa changamoto ya maji, kuanzia ufuatiliaji wa rasilimali fedha na utekelezaji wake,  ufuatiliaji wa maji lililoandaliwa na asasi ya Pakacha Group na kufadhiliwa na The Foundation For Civil Society, Elly Makala, Mkuu wa dawati la Elimu kwa Umma  (Takukuru ) Wilaya ya Kinondoni amesema ikiwa wananchi watatoa taarifa mapema , itakuwa ni rahisi kuchukua hatua mapema.

“Tutaokoa fedha nyingi za serikali zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ikiwemo miradi ya maji, Barabara na ujenzi wa vituo vya afya,” amesema Makala. Amesema takukuru ina majukumu mbalimbali, ikiwemo kutoa elimu ya madhara ya rushwa katika maendeleo ya nchi na wananchi wake. Hivyo ameongeza ni wajibu wa wananchi kushirikiana na viongozi kuanzia ngazi ya kata katika dhana nzima ya maendeleo, ikiwemo kuhoji mapato na matumizi ya miradi iliyomo maeneo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...