Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) imewataka Mawakala wa Forodha wote kuhakakisha wanafanya uhakiki wa namba zao za Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza na kuisaidia mamlaka hiyo kukusanya mapato mengi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Kamishna wa Kodi za Ndani wa mamlaka hiyo, Abdul Zuberi katika Semina iliyowakutanisha na makampuni ya mawakala wa forodha iliyojadili masuala mbalimbali ya kodi na ushuru wa forodha.

Amesema kuwa mawakala hao wanatakiwa kuhakiki TIN zao kutokana na kuwepo mkanganyiko kuwa na zaidi TIN hali inayowapa shida ya kutambua idadi ya mawakala wanaotakiwa kulipa kodi.“ Kuna watu wana TIN zaidi ya moja wanazitumia bila kufanyiwa uhakiki na wengine wanazifanyia udanganyifu inatupa tabu kuwatamabua hivyo ni vema mkazifanyia uhakiki,” amesema.

Amebainisha kuwa TRA mawakala watakaobainika kutumia TIN zaidi ya moja bila kuzifanyia uhakiki watachukuliwa hatua za kisheria.Amesisitiza kuwa mawakala wa forodha watakaofanya uhakiki wa TIN zao watapatiwa cheti cha utambulisho ili kuondokana usumbufu wakati wa kuwakagua.

Ameongeza kuwa mawakala wanatakiwa kuwasilisha taarifa sahihi za mapato yao kwa mwaka pamoja kulipa Kodi ya Ongezeko la Mapato (VAT).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...