Na Tiganya Vincent
HALMASHAURI  za Wilayani Mkoani Tabora zimetakiwa kutumia wataalamu na wanachuo wa Chuo cha Ardhi Tabora ili kuhakikisha vijiji na miji yao inapimwa na kupagwa kwa ajili ya kuwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi. Hatua hiyo itasaidia kuepusha migogoro miongoni mwa wananchi na pia kuwawezesha kutumia maeneo yao kujiletea maendeleo ikiwemo kukopa fedha katika Taasisi mbalimbali zinazotoa mikopo kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Kauli hiyo hiyo imetolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru wakati wa sherehe za mahafali ya 36 ya Chuo cha Ardhi Tabora.
Alisema Serikali imenunua vifaa mbalimbali vya kisasa kwa ajili ya Chuo hicho ambavyo vinawawezesha wataalamu wachche kupima eneo kubwa kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu ukilinganisha ambavyo wangetumia Kampuni binafsi.

Kabundunguru alisema hakuna sababu ya maeneo mbalimbali katika Halmashauri za Mkoa wa Tabora na mikoa jirani kuendelea kujengeka bila mpangilio wakati Chuo kipo karibu. Alisema upimaji wa maeneo ya mijini na vijiji Mkoani humo utasaidia kuwaondoa wananchi kuishi katika maisha magumu na hatarishi kutokana na maeneo yao kutokuwa katika mpangilio.
 Mkuu wa Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) Biseko Musiba(aliyesimama) akitambulisha wageni mbalimbali wakati wa mahafali ya 36 ya Chuo hicho yaliyofanyika jana mjini Tabora.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Ardhi Tabora(ARITA) Profesa Gabriel Kassenga akitoa salamu za Bodi wakati mahafali ya 36 ya  ARITA yaliyofanyika jana.
  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru akiwahutubia wahitimu wa mahafali ya 36 ya Chuo cha Ardhi Tabora jana.
 Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ardhi Tabora(ARITA) wakimsikiliza Mgeni rasmi wakati wa mahafali ya 36 ya Chuo hicho yalifanyika jana.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mathias Kabundunguru (mwenye Joho la bluu waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali na wakufunzi wa Chuo cha Ardhi Tabora jana mara baada ya kumalizika kwa mahafali ya 36 Chuo cha Ardhi Tabora yaliyofanyika jana. Picha na Tiganya Vincent

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...