Na Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania
Mahakama ya Tanzania iliingia mkataba na Shirika la Posta kuhakikisha kuwa huduma ya kusambaza nyaraka mbalimbali za Mahakama inatolewa kwa nchi nzima. Mkataba huu chini ya huduma mpya ya Posta mlangoni (The post at your door step) iliyoanzishwa na Shirika la Posta, umelipa jukumu la kukusanya na kusafirisha/kusambaza nakala za hukumu na nyaraka mbalimbali za Mahakama na kuzifikisha kwa wahusika kulingana na anuani zao na mahali walipo (Anuani za makazi).

Kwa kipindi kirefu kumekuwa na malalamiko miongoni mwa wananchi/wateja wa Mahakama juu ya usumbufu katika upatikanaji wa Nakala za hukumu na baadhi ya nyaraka za Mahakama, hali ambayo kwa namna moja au nyingine ilisababishwa kwa kutokuwa na taarifa sahihi za Mdaawa/Mteja na utaratibu stahiki wa ufikishaji wa nyaraka hizo. Mahakama ya Tanzania katika utekelezaji wake wa majukumu mbalimbali inawalenga wateja wake ili kuhakikisha haki inatolewa kwa wakati na kuimarisha imani ya Wadau kwa Mahakama. Utoaji wa huduma kwa wateja pamoja na mambo mengine unajumuisha utoaji wa nyaraka mbalimbali kama nakala za hukumu, wito wa kuitwa Mahakamani (Sumons).

Aidha; nyaraka muhimu zinazosambazwa kupitia huduma ya Posta Mlangoni ni Nakala za Hukumu ‘Judgment’, ‘Summons’ wito wa Mahakama, Mwenendo wa shauri/mashauri ‘Proceedings’, Maamuzi ‘Rulings’,  Amri ‘Order’, Tuzo ‘Award’/ ‘Decree’. Akizungumza kabla ya utiani saini wa mkataba huo Aprili, 2018, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Bw. Hussein Kattanga alisema kuwa hatua hii ni mwendelezo wa maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika ili kuwafikia wananchi kwa karibu zaidi.
 Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga (katikati) akitia saini Mkataba wa utoaji huduma ya Posta mlangoni (The post at your door step), anayeshuhudia kulia ni Msajili Mkuu- Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati aliyeketi kushoto ni Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Hassan Mwang’ombe, wanaoshuhudia (waliosimama) ni baadhi ya Viongozi/Maafisa kutoka Mahakama na Shirika la Posta.
Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Hassan Mwang’ombe akitia saini Mkataba huo.
Makabidhiano ya Mikataba hiyo mara baada ya kuhitimisha zoezi la utiaji saini. Kulia ni Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Bw. Hussein Kattanga na kushoto ni Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Hassan Mwang’ombe.
 Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati (kulia) akiongea jambo mara baada ya utiaji saini wa Mkataba huo.
(Picha na Mary Gwera, Mahakama)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...