Baraza la watoto la Taifa leo
limepata uongozi mpya baada kukamilisha uchaguzi wa Wajumbe wa Kamati
Kuu ya Taifa ya Baraza hilo na pia uchaguzi wa Mwenyekiti, Makamu wa
Mwenyekiti, Katibu na Mweka hazina wa Baraza hilo uchaguzi uliofanyika
jana katika Manispaa ya Singida.
Akiongea mara baada ya kutangaza
matokeo ya Uchaguzi huo Mwenyeliti wa Uchaguzi wa Baraza hilo Bi. Joyce
Mugambi amewataka viongozi wa Baraza hilo kufanya kazi kwa bidii ili
kuweza kukabiliana na changamoto zilizopo kwa kushirikiana na viongozi
wa Wizara Mama ili kuleta ufanisi kiutendaji.
Uchaguzi wa Viongozi wa Baraza
hilo ufanyika kila baada ya kipindi cha miaka miwili kwa kuwa na Wajumbe
kutoka Tanzania Zanzibar ambao kwa pamoja wanaunda wajumbe wa Baraza
Kuu la Baraza hilo ambapo Mwenyekiti na Makamu wake wanaweza kutoka
upande wowote wa Muungano, ikitokea mwenyekiti katokea Zanzibar inabidi
Makamu wake pia atokee huko ili Katibu atoke Tanzania Bara.
Viongozi walioshinda kwa nafasi
ya Mwenyekiti ni Johel Festo kutoka Mkoa wa Mwanza, Makamu Mwenyekiti
ni Aidath Ismail pia kutoka Mkoa wa Mwanza, Katibu ni Thuwaiba Abdallah
anayetokea Unguja Magharibi na viongozi hao utadumu kwa kipindi cha
miaka miwili.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya
Watoto wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Bw. Sebastian
Kitiku amemtaka Mwenyekiti mpya wa Baraza la Watoto Taifa kuhakisha
anaongeza idadi ya mabaraza katika ngazi ya Mkoa na Wilaya na kumtaka
kufanya hivyo kwa kushirikiana na Wizara ili kila mkoa upate uwakilishi
wake.
Wajumbe wa Baraza la Watoto Taifa wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii muda mchache kabla ya kuanza uchaguzi wa viongozi wa Baraza hilo Kitaifa.
Mmoja wa wasimamizi wa uchaguzi wa viongozi wa Baraza la Taifa la Watoto akikusanya kura kutoka kwa wajumbe wa Baraza wakati wa zoezi la kuwapigia kura wagombea wa uongozi wa Baraza la Taifa la Watoto.
Baadhi ya Wagombea wa uongozi katika Baraza la Watoto Taifa wakisubiri matokeo kujua kama bahati iko upande wao wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Baraza la Taifa la Watoto jana katika Manispaa ya Singida.
Viongozi wa nafasai nne za juu za Baraza la Taifa la Watoto wakiwa tayari kwa majukumu mapya wakawanza kushoto ni mweka hazina mpya wa Baraza hilo Ince Frank kutoka mkoa wa Mbeya, wa pili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo Aidathi Ismail kutoka Mkoa wa Mwanza na katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Taifa Joel Festo kutoka Mkoa wa Mwanza na kulia kwake ni Katibu wa Baraza Thuwaiba Abdallah kutoka Unguja Magharibi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...