Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye amewahakikishia wananchi wa baadhi ya vijiji ambavyo havina mawasiliano mkoani Lindi na Pwani kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli inahakikisha kuwa wananchi waishio kwenye vijiji hivyo wanapata huduma za mawasiliano ya uhakika

Nditiye ameyasema hayo akiwa kwenye ziara yake ya kukagua changamoto za hali ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa wananchi waishio maeneo ya Liwale, Lindi Vijijini, Mtama, Kibiti na Rufiji kwenye mkoa wa Lindi na Pwani baada ya kupata kilio kutoka kwa wabunge wanaowakilisha wanananchi wa maeneo hayo wakati wa kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania cha mwezi Novemba mwaka huu

Amesema kuwa Sekta ya Mawasiliano ni sekta inayoshika nafasi ya pili kwa kuchangia pato la taifa katika kipindi cha mwaka 2016/2107 kwa kiwango cha asilimia 13.1 ambapo mawasiliano yana changui kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa taifa letu na mawasiliano ndiyo kila kitu. “Wananchi mkiwasiliana kwa kununua vocha, kupiga simu na kutumia intaneti, Serikali inatoza kodi kidogo, ambayo wala haiumizi na wala mwananchi hausikii, lakini Serikali inapata mapato yake,” amesema Nditiye.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akifafanua jambo kwa wananchi wa kijiji cha Chihuta, Mtama mkoani Lindi kuhusu upatikanaji wa huduma za mawasiliano wakati wa ziara yake mkoani humo. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga.
 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (alyeinua mikono) akijadiliana na Mkuu wa Wilaya ya Liwale, Sara Chiwamba kuhusu upatikanaji wa mawasiliano kwenye kata ya Marui wakati wa ziara yake Wilayani humo ya kukagua ukosefu wa mawasiliano. Wa kwanza kulia mwenye kofia nyeupe ni Mbunge wa jimbo hilo Zuberi Kuchauka.
 Wananchi wa kijiji cha Chihuta, Mtama mkoani Lindi wakimuonesha Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Nditiye (hayupo pichani) namna wanavyotega mawasiliano kwenye simu zao wakati wa ziara yake ya kukagua changamoto za mawasiliano mkoani humo.
Wananchi wa kijiji cha Marui, Wilaya ya Liwale mkoani Lindi wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kukagua changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano mkoani humo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...