kumi ambao wamewekewa vifaa maalum vya kusaidia kusikia (Cochlear Implant) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo wameanza kusikia kwa mara ya kwanza baada ya kuwashiwa vifaa hivyo (switch on).

Watoto hao ambao wametoka katika mikoa mbalimbali nchini ikiwamo Dar es Salaam, Kilimanjaro, Tanga, Pwani na Ruvuma walifanyiwa upasuaji Novemba 12 hadi Disemba 16 mwaka huu ambapo zaidi ya asilimia 90 ya upasuaji huo ulifanywa na watalaam wa Muhimbili.Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Daktari Bingwa wa magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo amesema mbali na zoezi hilo la kuwawashia vifaa vya kusaidia kusikia, lakini pia watoto wengine ambao waliwekewa vifaa hivyo nao wamekuja kwa ajili kuangaliwa maendeleo yao na kupatiwa elimu ya kutunza mashine hizo.

Kwa mujibu wa Dkt. Liyombo, tangu kuanza kwa huduma hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Juni 2017 mpaka Disemba 2018, watoto 21 tayari wamewekewa vifaa hivyo ambapo jumla ya shilingi milioni 777 zimetumika kwa ajili ya upasuaji huo na endapo wangepelekwa kutibiwa nje ya nchi Serikali ingetumia shilingi Bilioni 2.1 kwa ajili ya kufanikisha matibabu hayo.Hivyo kutokana na upasuaji huo wa ubingwa wa juu kufanyika hapa nchini Serikali imeokoa shilingi Bilioni 1.3.

“Lengo la hospitali ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano ya kupunguza rufaa za wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi, kwani matibabu haya yanagharama kubwa kwani kupeleka mtoto mmoja nje ya nchi kwa ajili ya kupandikizwa kifaa cha usikivu ni shilingi milioni 100 wakati akipatiwa matibabu hayo Muhimbili hugharimu shilingi milioni 37 kwa mtoto mmoja,” amesema Dkt. Liyombo.
 
Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Edwin Liyombo akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuwawashia vifaa vya kusaidia kusikia kwa watoto 10 waliopandikizwa vifaa hivyo Novemba 12 hadi 16, 2018. Kutoka kushoto ni mtaalam wa usikivu, Fayaz Jaffer na Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo wa Muhimbili, Dkt. Aveline Aloyce .
????????????????????????????????????
Wazazi wa watoto wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Dkt. Liyombo kabla ya vifaa hivyo kuwashwa  tangu walipopandikizwa Novemba 12 hadi 16, 2018.
003
Mtoto Rehoboth Kivuyo akisikia kwa mara ya kwanza tangu wazazi wake walipobaini kwamba ana tatizo la kusikia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...