NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA
WAZEE wa dini ya Kiislamu jijini Mwanza wameushauri uongozi wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kumtanguliza Mungu, ukubali kukosolewa na kuacha kuwapokea mafisadi baada ya kupenyezewa bahasha.

Walitoa rai hiyo ilitolewa jana walipokutana na kuzungumza na Kaimu Sheikh wa Mkoa, Alhaji Sheikh Hassan Musa Kabeke ili  kutoa ushauri wao kwa viongozi wa BAKWATA Mkoa wa Mwanza.
Wazee hao walisema ili uongozi wa baraza hilo uende vizuri ukubali kukosolewa na zaidi wamtangulize Mwenyezi Mungu katika kutenda na kuwatumikia waislamu na kuwa wakweli.

“ Aliyewazidi  wenzake ni mcha Mungu na hivyo timu hii izidishe ucha Mungu.Msiwapokee mafisadi kwa kupenyezewa bahasha baada ya kuwa wamefanya ufisadi misikitini.Bahasha hizo zinaidhoofisha BAKWATA na kuonekana ni jalala,” alisema Sheikh Rajab Charahani.

Alisema yapo malalamiko katika misikiti mingi yakiwatuhumuwa viongozi wa wilaya kupokea bahasha ili kufumbia macho mambo ya ovyo na kuutaka uongozi wa BAKWATA Mkoa ujiepushe na bahasha hizo na wakubali kukoselewa ikizingatiwa kila binadamu anakosea na hata yeye (Charahani) alikosea, wakifanya hivyo wazee watawapa ushauri.
Sheikh Rajab Charahani mmoja wa wazee maarufu wa Dini ya Kiislamu jijini Mwanza akitoa nasaha kwa uongozi wa BAKWATA mkoani humu (hawapo pichani) baada ya kukutana kwenye kikao cha ushauri kilichofanyika jana katika Ukumbi wa Salum Ferej wilayani Nyamagana. Picha na Baltazar Mashaka
Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Alhaji Sheikh Hassan Musa Kabeke akizungumza na wazee maarufu wa dini ya Kiislamu jijini Mwanza (hawapo pichani) jana. Picha na Baltazar Mashaka 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...