Na  Karama Kenyunko Globu ya jamii.
SERIKALI  imesema hivi karibuni itahakikisha inamaliza kabisa tatizo kubwa la ukosefu wa maji katika Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani linatokana na ukosefu wa miundombinuz ya usambazaji.'
'
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa amesema hayo leo Desemba 18.2018 alipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maji Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani.
Waziri Mbarawa pia amewahakikishia wakazi wa Kiembeni, Kata ya Mapinga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani kuwa watapelekewa majisafi na salama na mpaka sasa tayari mradi utakaogharimu Sh. Bilioni 116 uko tayari na umeanza katika eneo hilo.

amesema, katika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama kwasasa uzalishaji wa maji kwa Mkoa wa Dar es Salaam umefikia lita bilioni 14 kwa mwezi.

Amesema kufuatia tatizo hilo la usambazaji ndio maana serikali kupitia mradi wake wa tanki la bagamoyo ulioanza mwaka jana iliamua kujenga tanki la maji la lita Bil. 6 ambalo litasaidia katika usambazaji kwa maeneo yote ya Bagamoyo na vitongoji vyake  ambao unatarajia kumalizika mwishoni mwa mwezi huu.

Waziri Mbarawa ameongeza kuwa, kwa siku jiji la Dar es Salaam lina uwezo wa kuzalisha lita milioni 502 za maji na mahitaji kwa mwezi ni lita bilioni 14, lakini changamoto ni usambazaji.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo juu mradi mkubwa wa maji wa ujenzi wa Tanki ambao utakapoisha utamaliza kero zote za maji Katika Wilaya ya Bagamoyo mjini na vitongoji vyake, wakati wa Wizara ya kukagua miradi ya maji Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani iliyofanyika leo Desemba 18.2018 mradi huo ulioanza mwanzoni mwa mwaka jana unatarajiwa kumalizika mwaka huu mwishoni. 


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...