Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama ameitaka Menejimenti ya Ofisi yake kushughulikia kero za watumishi kwa haki na usawa ili kumaliza kero zilizopo.

Ameyasema hayo wakati wa Mkutano na Watumishi wa ofisi ya Waziri Mkuu walipokutana kujadili masula yanayowakabili wawapo kazini uliofanyika Desemba 10, 2018 katika Ukumbi wa LAPF Dodoma.

Waziri aliwataka Watendaji wa ofisi yake kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili watumishi kuhusu madai mbalimbali ikiwemo; kupanda madaraja, uhamisho, usalama mahali pa kazi na masuala ya kuzingatia afya wawapo kazini ili kuhakikisha wanatekeeleza majukumu yao katika mazingira rafiki.

“Kama kuna motisha kubwa kwa mtumishi ni kumsaidia kutatua kero yake inayohusiana na utumishi wake kwa uzito unaolingana na tatizo au uhitaji wake ili kusaidia kuongeza morali yake katika kufanya kazi.”Alisema Mhagama.Sambamba na hilo waziri aliwaasa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kutumia mabaraza ya Wafanyakazi katika kujadili na kutatua kero wanazokabiliana nazo wawapo kazini.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiongoza kikao cha pamoja na Watumishi wa Ofisi hiyo walipokutana akujadili masuala yao ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na kuendelea kufanya kazi kwa umoja, mkutano huo ulifanyika Desemba 10, 2018 katika Ukumbi Mikutano wa LAPF Dodoma.
P2-min
Katibu Mkuu Ofisi yaWaziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi.Maimuna Tarishi akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
P6-min
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
P3-min  
Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia maelekezo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama  (hayupo pichani) wakati wa mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...