Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru amewaongoza watumishi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika Upimaji hiari wa Virusi Vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI na magonjwa mengine wakati wa Mafunzo maalum ya Afya katika mahali pa kazi, yaliyofanywa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma.

Magonjwa mengine yaliyofanyiwa upimaji ni pamoja na Kisukari, Shinikizo la damu (Pressure) na Uwiano wa Urefu na Uzito (Body Mass Index /BMI).

Akiongea na Watumishi wa Wizara katika Mafunzo hayo. Bwn. Kabundunguru alisema; “ Mafunzo ya Afya kwa Watumishi ni muhimu na yanalenga kuwapa uelewa zaidi na kuwawezesha Watumishi kupima Afya, kutambua hali za Afya zenu mapema na kuwawezesha kuishi kulingana na hali ya afya zenu huku mkiendelea kutoa huduma katika Utumishi wa Umma”.

Naye Afisa mwitikio wa Taasisi za umma (Public institutions response officer, Dkt. Hafidh Ameir kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS); Pamoja na mambo mengine, alieleza kuwa dhumuni Kuu pia la Mafunzo ni kuwaarifu watumishi wa umma kuhusu umuhimu wa kuchukua tahadhari ya magonjwa husika, hususani VVU na UKIMWI. Alisema; “ Watumishi wa umma wanasisitizwa kutambua kwamba mbali ya kuwa suala la afya dhaifu huathiri uwezo wao wa kufanya kazi kwa ufanisi, pia linawaathiri wao binafsi, hivyo watumishi wenyewe wanawajibika pia kujali afya zao.
kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru, akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala; Gideon Malabeja na Afisa Utumishi Mwandamizi; Joyce Mlowe katika ufunguzi wa Mafunzo Maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru akiwa kwenye zoezi la upimaji wa VVU/UKIMWI baada tu ya Mafunzo maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mathias Kabundunguru akiwa kwenye zoezi la upimaji wa Uwiano wa Urefu na Uzito (Body Mass Index /BMI) baada tu ya Mafunzo maalum ya Afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Timu ya Wataalam wa Afya kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ofisi za Wizara ya Ardhi – Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...