Na Yeremias Ngerangera…Bagamoyo.
Mfuko  wa hifadhi ya mazingira wa dunia (WWF-World  Wide  Fund for Nature)  unaendesha mafunzo  kwa viongozi wa jumuiya  za uhifadhi  kuwajengea uwezo wa  kuimarisha mawasiliano kati ya wanajumuiya na nje ya Jumuiya. Mafunzo hayo yanafanyika katika Hoteli ya Millenium sea breeze mjini Bagamoyo ambapo washiriki zaidi ya 48 kutoka mikoa ya lindi ,Mtwara, Pwani  na Ruvuma wanashiriki mafunzo hayo ya mawasiliano thabiti   kwa lengo la kujengewa uwezo wa kufanya mawasiliano na wananchi kwenye maeneo yao ya uhifadhi .

Akifungua mafunzo  hayo Drt  Severin Kalonga aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kujifunza mbinu, njia na namna ya kufanya mawasiliano na jamii zilizopo katika mazingira yao ili waweze kutoa ujumbe kwa jamii ukiwa sahihi kwa watu sahihi na kwa wakati sahihi na mwishowe kupatikana kwa matokeo chanya kwa wakati. Awali Drt Kalonga aliwaeleza washiriki wa mafunzo hayo namna WWF inavyofanya kazi katika kuhakikisha hifadhi zilizopo zinaendelea kutunzwa na kubaini njia pekee ya kuendelea kutunza hifadhi hizo ni kuendelea kutoa elimu ya uhifadhi kwa wananchi kwa kuwa na mawasiliano  yaliyorafiki na viongozi wao wa jumuiya.

Aidha  Kalonga aliwaambia washiriki hao kuwa upangaji wa matumizi bora ya ardhi yanaumuhimu mkubwa  katika jamii lakini akabainisha kuwa mbinu ,njia na namna ya kufikisha ujumbe kwa wananchi kwa viongozi wa jumuiya akazitiia mashaka.  Profesa Noah Sitati naye alisema katika uhifadhi wanakumbana na changamoto nyingi sana ikiwa ni pamoja na shughuli za kibinadamu kama kilimo na ufugaji kufanyika ndani ya hifadhi hivyo kuathiri wanyamapori na ukataji hovyo wa misitu.

 KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...