Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Benki ya
CRDB imekabidhi hundi ya shilingi Milioni 20 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa
Mwanza, Sekou Toure ili kusaidia ukarabati na ununuzi wa vifaa tiba katika wodi
ya upasuaji (Theatre) ya akina mama katika Hospitali hiyo.
Akizungumza
kwenye hafla fupi ya kukabidhi hundi hiyo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya
CRDB, Dkt. Joseph Witts alisema benki hiyo ni mdau mkubwa katika kuboresha huduma
za afya hapa nchini ambapo imekuwa ikitoa asilimia moja ya faida yake kwa ajili
ya kuwasaidia wananchi.
Mganga Mfawidhi
wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Dkt. Bahati Msaki aliishukru Benki ya
CRDB kwa mchango huo na kwamba utasaidia kuondoa changamoto ya utoaji huduma za
afya kwa akina mama.
Mbali na
hundi hiyo, pia Benki ya CRDB ilikabidhi luninga (TV) tatu za kisasa katika
Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa, Bugando
ili kutoa huduma kwa wananchi na wagonjwa wanaofika katika hospitali
hiyo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts akizungumza kwenye hafla hilo.
Baadhi ya watumishi wa Benki ya CRDB.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akipokea hundi ya shilingi Milioni 20 kutoka Benki ya CRDB. Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Katibu Tawala mkoani Mwanza, Dkt. Christopher Kadio, Mwenyekiti wa Bodi Hospitali ya Sekour Toure, Christopher Gachuma, Mganga Mkuu Hospitali hiyo, Dkt. Thomas Rotachunzibwa pamoja na watumishi wa Hospitali hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...