Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Benki ya CRDB imekabidhi hundi ya shilingi Milioni 20 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Sekou Toure ili kusaidia ukarabati na ununuzi wa vifaa tiba katika wodi ya upasuaji (Theatre) ya akina mama katika Hospitali hiyo.

Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi hundi hiyo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts alisema benki hiyo ni mdau mkubwa katika kuboresha huduma za afya hapa nchini ambapo imekuwa ikitoa asilimia moja ya faida yake kwa ajili ya kuwasaidia wananchi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Dkt. Bahati Msaki aliishukru Benki ya CRDB kwa mchango huo na kwamba utasaidia kuondoa changamoto ya utoaji huduma za afya kwa akina mama.

Mbali na hundi hiyo, pia Benki ya CRDB ilikabidhi luninga (TV) tatu za kisasa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Ziwa, Bugando  ili kutoa huduma kwa wananchi na wagonjwa wanaofika katika hospitali hiyo.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts akizungumza kwenye hafla hilo.
Baadhi ya watumishi wa Benki ya CRDB.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akipokea hundi ya shilingi Milioni 20 kutoka Benki ya CRDB. Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Katibu Tawala mkoani Mwanza, Dkt. Christopher Kadio, Mwenyekiti wa Bodi Hospitali ya Sekour Toure, Christopher Gachuma, Mganga Mkuu Hospitali hiyo, Dkt. Thomas Rotachunzibwa pamoja na watumishi wa Hospitali hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...