CHAMA Cha Mapinduzi wilaya ya Pangani kimemtunuku tunzo ya shukrani Rais John Magufuli kutokana na uwamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibuni .

Akikabidhi tunzo hiyo hapo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya wa Umoja wa wanawake wa chama hicho UWT Taifa Jesca Mbogo wakati akiwa katika ziara ya kukagua shughuli za maendeleo wilayani humo

Mwenyekiti CCM wilayani humo Hamis Mnegero alisema kuwa wameamua kutoa tunzo hiyo kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa Rais Magufuli kutoka na kufanikiwa kutekeleza ndoto ya siku nyingi ya kuwa na barabara ya kiwango cha lami wilayani humo.

“Tunajua kuna juhudi kubwa ambazo zilikuwa zimechukuliwa na marais waliotangulia lakini ndoto hizo hazikuweza kutimia lakini kwa juhudi kubwa za Rais wa awamu ya tani tumeona ujenzi huo sasa unakwenda kufanyika”alisema Mnegero.

Alisema kuwa barabara hiyo ilikuwa ni kilio cha muda mrefu kwa wananchi wa wilaya hivyo anaamini kwa kuanza kwa ujenzi huo kutaweza kufufua matumaini mapya kwa wilaya hiyo.

Kwa upande wake Naibu Katibu mbogo alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inajitahidi kuboresha mazingira bora katika sekta mbalimbali ili kuhakikisha kila mtanzania anapata fursa ya kupata maendeleo na unafuu wa maisha.

“Kama mnavyoona utekelezaji wa sera ya elimu bure pamoja na uboreshwaji wa huduma za afya hii yote ni kuhakikisha mtoto wa kitanzania anakuwa na afya bora lakini anapata fursa ya elimu bora”alisema Naibu Katibu huyo. 
Naibu Katibu Mkuu Mbogo yupo mkoani Tanga kwa ziara ya siku tatu kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali pamoja na kuzungumza na wanachama wa UWT mkoani hapa
 Mwenyekiti Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Pangani Hamis Mnegero akizungumza na waandishi wa habari hatua yao ya kumtunuku tunzo ya shukrani Rais John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibuni kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa
 Mwenyekiti Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Pangani Hamis Mnegero akizungumza na waandishi wa habari hatua yao ya kumtunuku tunzo ya shukrani Rais John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibuni kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa.
 Mwenyekiti Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Pangani Hamis Mnegero katikati akimkabidhi tuzo  ya shukrani ya  Rais John Magufuli ,Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kutokana na uwamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibuni kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah 
 Mwenyekiti Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Pangani Hamis Mnegero katikati akimkabidhi tuzo  ya shukrani ya  Rais John Magufuli ,Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kutokana na uwamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibuni kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah 
 Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kushoto akitazama tuzo aliyotunukiwa Rais Dkt John Magufuli ya Shukrani na  Chama cha Mapinduzi wilaya ya Pangani kutokana na uwamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibun katikati ni Mwenyekiit wa CCM wilaya ya Pangani Hamisi Mnegero kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah
 Naibu Katibu Mkuu wa UWT Taifa Jesca Mbogo kushoto akitazama tuzo aliyotunukiwa Rais Dkt John Magufuli ya Shukrani na  Chama cha Mapinduzi wilaya ya Pangani kutokana na uwamuzi wake wa kuridhia na kutia saini kuanza kwa ujenzi wa barabara ya Tanga Pangani hadi Bagamayo hivi karibun katikati ni Mwenyekiit wa CCM wilaya ya Pangani Hamisi Mnegero kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...