Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza watendaji wa Halmshauri zote nchini kutotumia wakandarasi katika kutekeleza miradi inayohusu Wizara bali kutumia mtindo wa 'Force Account' yani mafundi wa kawaida katika kutekeleza miradi hiyo.
Ametoa agizo hilo mkoani Ruvuma wakati alipotembelea na kujionea ukarabati na ujenzi katika Chuo cha Wauguzi Songea na Chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale katika ziara yake ya kikazi mkoani humo. Naibu Waziri huyo amefikia hatua hiyo baada ya kupokea taarifa ya kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa baadhi ya madarasa na ukuta wa Chuo cha Waganga mkoani humo ambao ungegharimu zaidi ya Shillingi 900 ambazo fedha hizo zingetumia mtindo wa 'Force Account' zingejenga zaidi madarasa hayo na ukuta.
Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa katika zama hizi za Serikali ya Awamu ya Tano itazingatia na kufuatilia matumizi sahihi ya fedha za miradi ya Maendeleo na yeye kama Naibu Waziri ataisimamia kwa karibu Miradi hiyo. Amesisitiza kuwa ujenzi wote wa miradi utakaohusu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii utazingatia utaratibu wa 'Force Account' na kibali cha wakandarasi kitatolewa na Mawaziri pekee na sio vinginevyo.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile akizungumza na baadhi ya wakufunzi, wafanyakazi na
wananfunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Mlale mkoani Ruvuma wakati
wa ziara yake chuoni hapo kujionea Ujenzi na Ukaratabi wa miundombinu
mbalimbali.
Baadhi
ya ya wakufunzi, wafanyakazi na wananfunzi wa wa Chuo cha Maendeleo ya
Jamii Mlale wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) wakati
wa ziara ya Naibu waziri huyo chuoni hapo kujionea Ujenzi na Ukaratabi
wa miundombinu mbalimbali.
Naibu
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile (katikati) akikagua mradi wa ujenzi wa chumba cha
pampu ya maji katika Chuo cha maendeleo ya Jamii Mlale unaogharinu
Shillingi Millioni 3 unaosimamiwa na Chuo cha Maendeleo ya Jamii na
Ufundi Misungwi katika ziara yake mkoani Ruvuma kulia ni Mkuu wa Wilaya
ya Songea Pololeti Mgema na Kushoto ni Mkuu wa chuo cha Maendeleo ya
Jamii Mlale Luciana Mvula
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile (katikati) akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha
Maendeleo ya Jamii Mlale mkoani Ruvuma wakati wa ziara yake chuoni hapo
kujionea Ujenzi na Ukaratabi wa miundombinu mbalimbali kulia ni Mkuu
wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema na Kushoto ni Mkuu wa Chuo cha
Maendeleo ya Jamii Mlale Luciana Mvula.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...