Hospitali
ya Kanda ya Bugando inatarajia kuajili Madaktari na wauguzi 13 kutoka
nchini Cuba katika kuhakikisha wanatoa huduma bora za afya kwa wananchi
kutokana na kuongeza idadi hiyo ya madaktari.
Akizungumza Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo amesema ziara yake katika hospitali Bugando ni kutokana ushirikiano uliopo kati ya Bugando na nchi ya Cuba.
Balozi amesema kuwa lengo ni kuangalia utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. Aidha amesema kuwa wanaendelea kushirikiana na hospitali hiyo katika maeneo mengine ambayo yana changamoto katika utoaji wa huduma za afya.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kanda Bugando Profesa Abel Makubi amesema kuwa Madaktari saba wanakuja mwezi ujao na wengine watakuja.
Amesema kuna ushirikiano wa karibu kati ya hospitali ya Bugando na Cuba hivyo wanatarajia kupata mengi katika nchi hiyo.
Profesa Makubi mesema Madaktari wataokuja Madaktari Bingwa wa Mfumo wa Mkojo,Koo-pua na masikio (ENT),Wataalamuwa usingizi ,mionzi,na madaktari bingwa wa huduma za dharula pamoja na madaktari bingwa wa magonjwa ya ubongo na uti wa mgongo.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akitia saini kitabu cha wageni katika hospitali ya Kanda ya Bugando jijini Mwanza wakati alipotembelea hospitali hapo akiwa na familia yake.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akizungumza na menejimenti ya Hospitali ya Bugando wakati alipofanya ziara akiwa familia yake ikiwa na mahusiano yaliyopo katika ya hospitali nan chi ya Cuba.
Akizungumza Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo amesema ziara yake katika hospitali Bugando ni kutokana ushirikiano uliopo kati ya Bugando na nchi ya Cuba.
Balozi amesema kuwa lengo ni kuangalia utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. Aidha amesema kuwa wanaendelea kushirikiana na hospitali hiyo katika maeneo mengine ambayo yana changamoto katika utoaji wa huduma za afya.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Kanda Bugando Profesa Abel Makubi amesema kuwa Madaktari saba wanakuja mwezi ujao na wengine watakuja.
Amesema kuna ushirikiano wa karibu kati ya hospitali ya Bugando na Cuba hivyo wanatarajia kupata mengi katika nchi hiyo.
Profesa Makubi mesema Madaktari wataokuja Madaktari Bingwa wa Mfumo wa Mkojo,Koo-pua na masikio (ENT),Wataalamuwa usingizi ,mionzi,na madaktari bingwa wa huduma za dharula pamoja na madaktari bingwa wa magonjwa ya ubongo na uti wa mgongo.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akitia saini kitabu cha wageni katika hospitali ya Kanda ya Bugando jijini Mwanza wakati alipotembelea hospitali hapo akiwa na familia yake.
Balozi wa Cuba nchini Tanzania Profesa Lucas Polledo akizungumza na menejimenti ya Hospitali ya Bugando wakati alipofanya ziara akiwa familia yake ikiwa na mahusiano yaliyopo katika ya hospitali nan chi ya Cuba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...