*Wengi ni wanafuzi katika mikoa ya Tanga,Morogoro na Dodoma

Na Chalila Kibuda , Globu ya Jamii

Idadi ya abiria katika kituo cha mabasi Ubungo imeendelea kuongezeka kwa kwa sehemu kubwa wakiwa wanafunzi.

Akizungumza na Michuzi Blog Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria Hassan Mchanjama amesema kuwa abiria katika kituo cha Ubungo ni kubwa lakini wanasafiri kutoka na baadhi daladala kupata vibali.

Amesema abiria wengi ni mikoa ya Tanga, Dodoma pamoja na Morogoro ikiwa sehemu kubwa abiria hao ni wanafunzi.

Mchanjama amesema abiria wanavyofika katika kituo cha mabasi Ubungo wakate tiketi ndani ya Kutuo.Mmoja wa abiria Hamis Seif amesema kuwa kuna changamoto ya Usafiri katika msimu wa siku kuu na kuomba yaongezwe mabasi hata daladala katika mikoa ya jirani na Dar es Salaam.

Aidha amesema kuwa suala la ukaguzi katika kituo cha mabasi Ubungo ni mzuri na kutaka na mikoa mingine wafanye hivyo kwa ajili ya usalama wa abiria.
 Askari wa usalama barabarani Grant Pawa akiandika makosa ya basi wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Moja ya tiketi aliyekatiwa msafiri ambaye kampuni ya basi hilo halipo katika kituo cha Ubungo abiria anadai kuwa aliyemkatia na kutia saini ni Rama Tall.
 Abiria wakiwa wamefurika katika katika Kituo cha Mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika kituo cha mabasi Ubungo wakiwa na fundi wakufanya ukaguzi wa basi katika kituo cha mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nuru Hussein akifanya Ukaguzi katika basi kuangalia uimara wa Gurudumu pamoja na Brenk katika kituo mabasi Ubungo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...