KAMPUNI
Ya usafirishaji abiria ya Moovn Driver kwa kushirikiana na umoja wa
madereva wa mtandao (TODA), leo wametoa msaada wa vyakula na mavazi kwa
kituo cha watoto yatima cha Maunga kilichopo Hananasifu, Kinondoni,
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu wa Umoja wa Madereva wa Mtandao (TODA), Fredy Peter, amesema kuwa msaada huo umelenga kuwapatia nafuu katika mazingira waliyomo na akatoa wito kwa makampuni na taasisi zingine ziige mfano huo kuwasaidia watu wenye mahitaji, hasa watoto wanaoishi kwenye vituo vya mayatima.
Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu wa Umoja wa Madereva wa Mtandao (TODA), Fredy Peter, amesema kuwa msaada huo umelenga kuwapatia nafuu katika mazingira waliyomo na akatoa wito kwa makampuni na taasisi zingine ziige mfano huo kuwasaidia watu wenye mahitaji, hasa watoto wanaoishi kwenye vituo vya mayatima.
Baadhi ya wawakilishi kutoka kampuni ya usafirishai abiria ya Moovn
Driver wakishirikiana na umoja wa madereva wa mtandao (TODA), wenye
T-shirt nyeusi, wakimkabidhi msaada mwanamama Zainab Bakari ambaye ni
mlezi wa kituo cha watoto yatime cha Maunga cha Hananasifu, Kinondoni,
Dar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...