Ni kama zimepita siku kumi tu lakini tayari leo imetimia miaka 10 tangu Mpendwa wetu Cassian Kigeso Malima ulipotutoka ghafla jioni ya tarehe 9 Januari 2009 katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam na kupumzishwa katika kwenye makaburi ya Mwisenge, Musoma mjini tarehe 14 Januari 2009.

Muongo mmoja umepita lakini ungali unaishi kiroho maishani mwetu na tunajenga taswira ungekuwa na mwonekano gani, ungekuwa na madaraka gani na mengine mengi yanayoeleza mafanikio ya duniani. Hatuna budi kumshukkuru Mungu kwa zawadi ya uhai wako na  mapenzi yake yatimizwe.

Baba, wanao, ndugu, majirani na rafiki zako daima tutaendelea kukukumbuka kwa upole, ucheshi na uchapakazi wako wakati wa uhai wako, haiba ambayo haikubanduki kila tunapokukumbuka.

Tunamuomba Mungu wa Rehema aendelee kukupumzisha kwake katika amani ya milele tukiamini tutaonana siku ya mwisho. Amina.

1 Wathesalonike 4:13-14 (Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...