Ni kama zimepita siku kumi tu lakini
tayari leo imetimia miaka 10 tangu Mpendwa wetu Cassian Kigeso Malima
ulipotutoka ghafla jioni ya tarehe 9 Januari 2009 katika hospitali ya Aga Khan,
Dar es Salaam na kupumzishwa katika kwenye makaburi ya Mwisenge, Musoma mjini
tarehe 14 Januari 2009.
Muongo mmoja umepita lakini ungali
unaishi kiroho maishani mwetu na tunajenga taswira ungekuwa na mwonekano gani,
ungekuwa na madaraka gani na mengine mengi yanayoeleza mafanikio ya duniani.
Hatuna budi kumshukkuru Mungu kwa zawadi ya uhai wako na mapenzi yake yatimizwe.
Baba, wanao, ndugu, majirani na rafiki
zako daima tutaendelea kukukumbuka kwa upole, ucheshi na uchapakazi wako wakati
wa uhai wako, haiba ambayo haikubanduki kila tunapokukumbuka.
Tunamuomba Mungu wa Rehema aendelee
kukupumzisha kwake katika amani ya milele tukiamini tutaonana siku ya mwisho. Amina.
1
Wathesalonike 4:13-14 (Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao
waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...