Leo (21-01-2019), mahojiano ya Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki, alipelekwa kuhojiwa katika kipindi maarufu cha BBC cha HARDtalk, jijini London.

Katika mahojiano hayo, Mtangazaji alionekana kujiandaa vizuri baada ya kuchimbua taarifa zinazomhusu Tundu Lissu na utendaji wa Raisi John Pombe Joseph Magufuli, ambao ulionekana kumkuna mtangazaji.

Watoto wa mjini wangesema, ama kweli Mbunge huyo mropokaji, ameingia choo cha kike. Mtangazaji alichimbua na kujiridhisha, ili asije akavunja heshina ya BBC kwa uchochezi na madai ya kufikirika yasiyokuwa na chembe ya ushahidi.

Katika siku ambazo Tundu Lissu hatazisahau, basi ni leo. Angekuwa katika masuala ya dini, leo alistahili kuokoka.

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR: Wewe ni mwanasheria mwandamizi. Unaifahamu Sheria vizuri kuliko mimi. Ni hatari sana kukurupuka na kudandia mambo serious pasipokuwa na uthibitisho au ushahidi thabiti wa unayoyasema. Baadhi ya watu unaowatuhumu ni wapinzani wenzio na misimamo yao inakinzana na kukanusha madai yako kabisa.

LISSU: Wapigie simu.

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR: Mfano Lawrence Masha aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Serikali ya Kikwete, badae akahamia upinzani na kuwa mpinzani mkubwa wa Rais Magufuli, baada ya kuridhishwa na utendaji wa Rais Magufuli, sasa anamkubali Sana. Anasema, japokuwa huwezi kukubaliana na kila jambo analofanya Magufuli, lakini dhamira yake na utendaji wake unagusa maisha ya watanzania wengi, hasa wale wa kawaida.

Madai yako ni ya kuunga unga, (allegations, connections, claims using inflammatory language) pasipokuwa na ushahidi wa kuhusika kwa serikali katika shambulio lako.

Lissu: Kwasababu nilikuwa nafuatiliwa na watu.

MTANGAZAJI akapigwa butwaa.

Mbona inaweza kuwa mtu yeyote mbaya katika jamii aliyemuudhi? Wewe ulikuwa mnadhimu wa upinzani Bungeni, ulikuwa Rais wa TLS na mpinzani maarufu. Ingeweza kuwa mtu yeyote. Una uthibitisho gani wa madai yako?

LISSU: Siku hiyo hapakuwa na walinzi getini. 

(Mtangazaji anazidi kumshangaa na madai yasiyokuwa na chembe ya ushahidi). 

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR:

Mbona Rais Magufuli alilaani tukio la kushambuliwa kwako na akaagiza uchunguzi ufanyike Mara moja.

LISSU: Rais Magufuli kamwe hajasema lolote kuhusu hilo shambulio. Lakini, alituma ujumbe wa twita haraka haraka halafu ukapotea.

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR:

Lakini ulienda mbali sana kumuita Rais wako dikteta uchwara, hivi kweli angekuwa mbaya hivyo, Magufuli angekubalika na watu wengi Tanzania, asilimia 70 na wengi ndani na nje ya Tanzania wanathibitisha kuwa anafanya kazi nzuri sana.

Magufuli ameondoa wafanyakazi hewa, ambayo ilikuwa wizi na rushwa na hili sio jambo dogo kwa nchi za kiafrika, anatekeleza ahadi zake vizuri, ameongeza makusanyo ya kodi na kufanya maendeleo makubwa hadi Tanzania inakuwa mfano, ameongeza ufanisi na uwajibikaji katika Serikali na jamii. Mwingereza mmoja was Oxford ameandika kuwa Magufuli ameweza kuutafuna mfupa uliowashinda wengi kwamba Taifa la kiafrika haliwezi kushindana na mashirika makubwa ya kimataifa na likashinda, lakini Magufuli ameweza kwenye sekta ya madini. 

Wewe katika upinzani huyapendi hayo mafanikio? (Akagongwa)

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR: Lakini lugha yako ni ya kuudhi, unatoa madai bila kuwa na ushahidi, je lugha yako ya kuudhi itachochea moto au itapoza joto la mifarakano?

· Umesema 2020 umedhamiria kupambana na Magufuli katika uchaguzi mkuu, utatumia mkakati wa kigomvi au njia ya amani?

· Sasa unamtuhumu Magufuli kwa mambo mengi mabaya (hata kwa mazuri yanayoonekana). Uko tayari kurudi nyumbani Tanzania kupambana na Magufuli?

LISSU: Hadi nitakapopona. Madaktari wakisema niko fiti tu, kesho yako nitapanda ndege kurudi (Mtangazaji anamtazama kama anachosema ni kweli)

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR: Utakuwa na ulinzi wowote?

LISSU: Serikali itanilinda saa 24. (Mtangazaji akamstukia kama ni mzima. Kweli mlinzi wako ndiye utajaribu kumkandia hivyo).

MTANGAZAJI STEPHEN SACKUR: Utalinda haki za mashoga na wanafunzi wa shule za msingi wasome wakiwa na mimba?

LISSU: Mashoga wana haki ya kutoingiliwa vyumbani mwao. Wana haki ya usiri. Wasichana wenye mimba wataendelea na shule.


FIKIRIA BINTI YAKO YUKO DARASANI KATIKA SHULE YA MSINGI, PEMBENI WASICHANA WENZAKE 10 NI WAJAWAZITO, WAVULANA 15 NI MASHOGA. MWANAO ATAKUWA SALAMA? BASI UJUE HUYU JAMAA MGONJWA.

MTANGAZAJI AMEMUUMBUA. KUMBE AMEKARIRI SHERIA TU. LEO BBC IMEMUUMBUA. KUMBE NI KIMEO. “HIVI KWELI MAFANIKIO HAYA YA MAGUFULI WEWE HUYATAKI,” MTANGAZAJI ALIPOMUULIZA, LISSU KAMBADILISHIA MADA.

KALAGHABAHO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...