Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SHEIKH wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum amesema Spika wa Bunge akimuita mtu lazima aende.

Ametoa kauli hiyo leo Januari 18,2019 mbele ya Rais Dk.John Magufuli wakati wa hafla ya makabidhiano ya Mfumo wa Kuratibu na kudhibiti Mawasiliano(TTMS) yaliyofanyika Mamlaka yaMamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA).

Sheikh Alhad wakati anaomba dua kwa ajili ya viongozi wa ngazi mbalimbali nchini alianza kwa kumuombea Rais Magufuli, Makamu wa Rais Samoa Suluhu Hassan ,Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Spika wa Bunge.

"Mwenyezi Mungu tunakuomba uumpe afya njema Spika wetu wa Bunge mzee Ndugai.Huyu Spika akimuita mtu lazima aende," amesema Sheikh Alhad huku baadhi ya watu waliokuwa wanasikiliza dua yake kuanza kucheka.

Haikufahamika mara moja walikuwa wanacheka nini lakini ukweli kauli ya Sheikh Alhad inakuja kipindi ambacho kunamjadala baada Spika Ndugai kumuita Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG)Profess Mussa Assad katika Kamati ya Bunge ya Kinga,Haki na Maadili ili ahojiwe baada ya kuelezea Bunge ni dhaifu.

Hata hivyo wakati Sheikh Alhad akisema kwamba mtu akiitwa na Spika Ndugai lazima aende inakuja kipindi ambavyo tayari CAG Profesa Assad amethibitisha ataitikia mwito wa Spika Januari 21 mwaka huu.

Kwa upande wa Spika jana wakati anazungumza na waandishi wa habari amesema ana uhakika Profesa Assad atakwenda kwenye kamati kuhojiwa ili apate fursa ya kuwasilisha utetezi wake na kwamba iwapo hatafika atajua nani muajiri wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...