Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
MWANAMKE mmoja nchini Misri amefukuzwa chuo baada ya kuonekana akimkumbatia mwanaume katika moja ya video iloyosambaa katika mitandao.

Binti huyo amefukuzwa katika chuo cha Al -Azhar akishutumiwa kujidharilisha yeye na chuo baada ya kuonekana akimkumbatia mwanaume huyo katika video ambayo ilichukuliwa katika chuo cha Mansoura nchini humo.

Baraza la nidhamu la chuo cha Al- Azhar lililokaa siku ya jumamosi liliamua kumfukuza Chuo binti huyo, Msemaji wa baraza hilo Ahmed Zarie alieleza vyombo vya habari.

Imeelezwa kuwa video hiyo imeleta picha mbaya kwa chuo hicho kitu ambacho hakiruhusiwi aidha imefahamishwa kuwa kukumbatiana baina ya mwanamke na mwanaume ambao hawajaolewa sio maadili wala taratibu za jamii ya taifa hilo.

Kwa upande wa kijana aliyeonekana kwenye video, msemaji wa baraza hilo amesema kuwa watakaa leo jumatatu na kufanya maamuzi dhidi yake. 

Chanzo: Daily Mail

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...