Na Munir Shemweta, Dodoma
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa ofisi za wizara katika mji wa serikali ya Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Dk Mabula alitoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari 2019 wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo liko chini ya Wizara yake.
Alisema kazi inayofanywa na shirika la Nyumba la Taifa kujenga ofisi za Serikali katika mji huo kwa sasa unaenda kwa kasi na unatia moyo jambo linalooonesha kuwa mradi wa ujenzi wa ofisi hizo utakamilika katika muda uliopangwa.
Katika mradi huo Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia kampuni yake ya ujenzi inajenga ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Aidha, Dk Mabula amefurahishwa na ufuatialiaji wa ujenzi wa ofisi hizo unaofanywa na Wizara ya Fedha pamoja na Viwanda na Biashara na kueleza kuwa hatua hiyo inalifanya Shirika hilo kufanya kazi kulingana na mahitaji ya wateja wake.
Alibainisha kuwa, pamoja na changamoto ya kukatika umeme lakini NHC imejitahidi na kilichomfurahisha ni kuwepo vifaa vyote vya ujenzi kwenye eneo la ujenzi jambo linalompa faraja kuwa hakuna kitakachokwamisha ujenzi kukamilika kwa wakati
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amepongeza jitihada znazofanywa na Rais John Pombe Magufuli za kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Dodoma na kubainisha kuwa hatua hiyo inatimiza ndoto ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Emma Lyimo alilisifu Shirika la Nyumba la Taifa kwa kasi kubwa wanayoendelea nayo kwenye ujenzi wa ofisi ya Wizara yake na kubainisha kuwa pamoja na kuchelewa kuanza ujenzi lakini kasi wanayoenda nayo ana imani ujenzi utakamilika kwa wakati.
Naye Msimamizi wa ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo la Makazi Mhandisi Grace Musita alisema, ujenzi wa ofisi umefikia asilimia sabini na tano na anatarajia utakamilika katika tarehe iliyopangwa kwa kuwa wamefikia hatua nzuri ya kukamika.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiangalia maendeleo ya Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na katikati ni meneja mradi Haikameni Mlekio.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akioneshwa moja ya kifaa kitakachotumika katika Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kulia ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na kushoto ni meneja mradi Haikameni Mlekio.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Bisahara Emma Lyimo (Kulia) wakati alipotembelea maendeleo ya Ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Hassan Mohamed.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiongozwa na Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali eneo la Mtumba Dodoma .
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula katikati akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali wa Mtumba kutoka kwa meneja mradi wa Shirika la Nyumba Haikameni Mlekio wakati alipofanya ziara, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita.
  Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali wa Mtumba kutoka kwa meneja mradi wa Shirika la Nyumba Haikameni Mlekio (kulia) wakati alipofanya ziara, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...