Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ametengua uteuzi wa Makamandaa
wa polisi watatu wa mikoa ya Temeke,Ilala, na Arusha kwa makosa
mbalimbali ikiwemo kujihusisha na vitendo vya Rushwa kulinda Askari
wanaohusishwa katika kusindikiza utoroshwaji wa Bidhaa, na madawa ya
kulevya.
Lugola ametaja Makamanda hao kuwa ni Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Emmanuel Lukula na Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi
Waziri Lugola ametangaza uamuzi wake huo leo Jumatano Januari 16, 2019, katika mkutano na waandishi wa habari akibainisha kuwa amefanya hivyo baada ya kushauriana na vyombo anavyoviongoza.
Lugola pia amemtaka Kamanda Wa kikosi cha Usalama barabarani nchini kujitathmini kama anatosha katika nafasi hiyo. "Mimi ndio waziri wa mambo ya ndani ya nchi nasimamia vyombo vyote hivyo, nikitengua uteuzi inabaki kazi ya IGP kuteua mtu mwingine kujaza nafasi" amesema waziri Kangi Lugola.
Lugola ametaja Makamanda hao kuwa ni Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Emmanuel Lukula na Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi
Waziri Lugola ametangaza uamuzi wake huo leo Jumatano Januari 16, 2019, katika mkutano na waandishi wa habari akibainisha kuwa amefanya hivyo baada ya kushauriana na vyombo anavyoviongoza.
Lugola pia amemtaka Kamanda Wa kikosi cha Usalama barabarani nchini kujitathmini kama anatosha katika nafasi hiyo. "Mimi ndio waziri wa mambo ya ndani ya nchi nasimamia vyombo vyote hivyo, nikitengua uteuzi inabaki kazi ya IGP kuteua mtu mwingine kujaza nafasi" amesema waziri Kangi Lugola.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...