Kampuni inayoongoza ya mauzo ya moja kwa moja QNET, na mbia katika ligi ya mabingwa ya CAF, Kombe la Shirikisho la CAF na kombe la Super Cup imewapongeza Shirikisho la Soka Afrika, CAF na vilabu vyote vinavyoshiriki katika mashindano yote ya klabu ya CAF mwaka 2019. 

QNEt imekaribisha ushirikiano wake na CAF, katika mwaka 2018 na inaelezea fahari yake katika mpira wa miguu wa Afrika. 

Ushirikiano kati ya kampuni ya QNET na CAF ni sehemu ya juhudi za QNET za kukuza michezo Afrika na dunia kote.Kwa kweli, kama ilivyo katika michezo, QNET inaongozwa na ari ya kufanya kazi kwa pamoja kama timu pamoja na shauku wakati inapofanya biashara zake kila siku. 

Ushirikiano huu ni fursa nyingine kwa QNET kuwa karibu na wawakilishi wake wa kujitegemea (IRs), walaji na wateja ambako QNET inaendesha shughuli zake tangu zaidi ya muongo mmoja iliopita. 

Meneja Mkuu wa QNET wa Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara, Biram Fall amesema kwamba, “Mwaka uliopita ulikuwa ni mwaka mzuri kwa mpira wa miguu barani Afrika. Katika QNET tunaona fahari sana kujihusisha na CAF na ukuaji wa mchezo wa mpira wa miguu barani. Falsafa ya biashara yetu inashikilia mwenendo wa mpira wa miguu, ambao kimsingi ni ufanyaji wa kazi katika timu, ushirikiano, shauku na kufanyakazi kwa bidii. 

Tunawawezesha wajasiriamali katika bara zima la Afrika na tumejikita katika kusaidia wengi zaidi waweze kufanikiwa. Vilevile ni heshima kwetu kudhamini mashindano haya maarufu na yanayoheshimiwa sana, na tusingeweza kupata mshirika bora zaidi kuliko Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kuweza kufanikisha lengo hili. Mwaka 2019 unaonekana kutia matumaini zaidi na QNET itakuwa katika upande wa CAF kwaajili ya kuhakikisha utendaji bora zaidi”. 

Katika mwaka 2019, QNET itakuwepo zaidi viwanjani ikiwa na uhamasishaji, matukio zaidi kwaajili ya kuhamasisha mashabiki kuongeza nguvu kazi ya mauzo ya QNET na wawakilishi wa kujitegemea (IRs). 

QNET inaendelea kuongeza uwepo wake katika bara zima la Afrika, ikiwa inatoa fursa za ujasiriamali kwa watu na kusaidia watu kubadili historia zao vyema zaidi. Ukiachilia mbali ushirikiano wa kimichezo, QNET pia ni kampuni ambayo inajihusisha na majukumu ya kijamii, kutoa kwaajili ya maendeleo endelevu ya jamii katika kanda zote ambako inaendesha shughuli zake. Katika mwezi Novemba, kampuni ya QNET ilitunikiwa tuzo ya mwaka ya e-commerce CSD Company na Kituo cha Uwajibikaji kwa Jamii cha Afrika Magharibi (Centre for Corporate Social Responsibility West Africa).
Pichani kulia shoto ni Meneja Mkuu wa QNET wa Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara, Biram Fall akiwa na mchezaji bora  (Afrika) wa zamani 20o1 kutoka nchini Senegal El Hadj Diouf

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...