Na Nyamagory Omary wa PMO
Serikali kupitia Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imezipa Kandarasi ya thamani ya shilingi 2.9 bilioni kampuni tatu za vijana wa Kitanzania ili kutekeleza mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House). 
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana Mhe.Anthony Mavunde wakati akizindua mafunzo hayo  Januari 05, 2019 yanayoendelea katika Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro. 
Programu hiyo ambayo itatumia jumla ya shilingi 2.9bilioni katika utekelezaji wake ambapo kampuni zilizoshinda kandarasi hiyo ni Kampuni za vijana wazalendo wa kitanzania ambao ni wabobezi katika masuala ya kilimo ikiwemo kampuni na Royal Agriculture Ltd, Holly Agriculture  Group Ltd, na SUGECO. 
Mafunzo haya yatafanyika katika Mikoa yote Tanzania Bara na kuhakikisha Halmashauri 84 zinafikiwa kwa awamu hii ya kwanza lengo likiwa ni  kuwajengea vijana ujuzi kupitia kilimo cha kisasa ambapo tayari kwa mwaka huu wa fedha imeanza mafunzo hayo  kwa kutumia teknolojia ya Kitalu Nyumba (greenhouse). 
“Kwa kuanzia tutahakikisha kila Halmashauri tunatoa mafunzo kwa vijana 100 na kati yao vijana 20 watapatiwa mafunzo ya kujenga Vitalu Nyumba ili kwa wale watakaopenda kuendelea na kilimo hiki wasikose wataalamu wa kuwajengea Vitalu hivyo ”alisisitiza Mavunde. 
Aidha, Amewataka vijana kutumia fursa ya kilimo katika kujikwamua na changamoto za ajira na kuelezea umuhimu wa kilimo katika kuongeza pato la Taifa na kuchangia katika uchumi wa viwanda nchini.

 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na mtaalamu wa masuala ya kilimo cha kisasa kwa  kutumia mabwawa ya samaki (Acquculte) alipotembelea kukagua mradi huo, wa kwanza kulia ni Naibu Waziri Ofisi hiyo Mhe Stella Ikupa
 Manaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu wakiangalia kiazilishe katika moja ya banda la maonesho la vijana walioshiriki mafunzo ya Kilimo cha kisasa cha kitalu nyumba. Katikati ni Mhe.Stella Ikupa anayeshughulikia Wenye Ulemavu na Kushoto ni Mhe.Anthony Mavunde (Kazi, Vijana na Ajira).

 Baadhi ya viongoizi wakishuhudia Naibu Waziri Ofisi ya Waziri (Wenye Ulemavu) Mhe.Stella Ikupa akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Muongozo wa masuala ya kilimo cha Kitalu Nyumba wakati wa warsha hiyo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akikagua biskuti zilizotengenezwa kwa kutumia nanasi ikiwa ni moja ya bidhaa zilizotengenezwa na vijana waliopewa mafunzo na SUGECO wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO Bw.Revocatus Kimario .
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akiangalia mapapai yaliyolimwa kwa njia ya kisasa katika mashamba ya SUGECO katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...