Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Tumaini Magessa amezindua utoaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo kwa kuwataka wafanyabiashara wakubwa na wakati kutojihusisha na zoezi hilo.  Magessa aliyasema hayo mji mdogo wa Mirerani, wakati wa kugawa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo.

Magessa alisema wafanyabiashara waliosajiliwa kwenye mfumo wa mamlaka ya mapato nchini (TRA) hawapaswi kupatiwa vitambulisho hivyo. "Serikali ipo pamoja nanyi wafanyabiashara wadogo, ndiyo sababu Rais John Magufuli akawatambua na kuagiza vitambulisho vyenu vitengenezwe," alisema Magessa. 

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Yefred Myenzi alisema wafanyabiashara wanapaswa kuwa wazalendo kwa kulipa kodi ili kufanikisha maendeleo. "Kupitia kodi ndiyo serikali inafanikisha maendeleo mbalimbali ikiwemo kujenga vyumba vya madarasa yahoo shule za sekondari na msingi ambavyo watoto wetu watasoma," alisema  Myenzi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Yefred Myenzi akizungumzia umuhimu wa ulipaji kodi kwa wafanyabiashara wakati wa uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo wilayani humo.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Zuwena Omary akielezea namna ya upatikanaji wa vitambulisho hivyo wakati wa uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo wilayani humo.
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mhandisi Tumaini Magessa akielezea sifa za wafanyabiashara wadogo wanaopaswa kupata vitambulisho hivyo vilivyotolewa na Rais John Magufuli. 
Wafanyabiashara wadogo wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara wakifuatilia kikao cha Kaimu Mkuu wa Wilaya hiyo mhandisi Tumaini Magessa wakati wa uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogowadogo wilayani humo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...