Wachezaji wa timu ya Bandari wakishangilia baada ya kufanikiwa kupata goli lililowapelekea hatua ya nusu fainali ya Michuano ya Sportpesa leo katika Uwanjwa wa Taifa Jijini Dar es Salaam.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

TIMU ya Singida United ya Tanzania imepoteza mchezo wake wa hatua ya robo fainali kwa kufungwa goli 1-0 dhidi ya Bandari uliochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.


Mchezo huo ulioanza majira ya saa 8 mchana ukiwa  ni mechi ya Ufunguzi wa michuano ya Sportpesa inapoteza dhidi ya Bandari na kupunguza idadi ya wawakilishi kutoka Tanzania. mashindano hayo.

Singida United imepoteza mchezo huo na inakuwa ni timu ya kwanza kuondolewa kwenye hatua ya robo fainali kutoka Tanzania na kuifanya Bandari kufanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali.


Mchezo unaoendelea kwa sasa ni kati ya Yanga na KK Sharks Uwanja wa Taifa ili kumpata mshindi atakayetinga hatua ya nusu fainali ya mashindano haya.

Mshindi wa SportPesa Cup atapata fursa ya kucheza na timu ya Everton ambayo nayo inadhaminiwa na kampuni ya SportPesa na msimu huu mshindi atafuatwa nyumbani na Everton wenyewe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...