Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa (APNAC) pamoja na wawezeshaji wa semina (hawapo kwenye picha), wakati wa semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma. 
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akifungua semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika (wa pili kushoto) wakati wa semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma. Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph kakunda na kushoto ni Katibu wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa, Mhe. Daniel Mtuka
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Cpt. George Mkuchika wakati wa semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma. 
Afisa Mtendaji Mkuu wa wakala wa vipimo na mizani, Dkt. Ludovick Manenge akizungumza na wajumbe wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa (APNAC) wakati wa semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma. 
Mjumbe wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa (APNAC) na Mbunge wa Mufundi, Mhe. Cosato Chumi akizungumza jambo wakati wa semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma. 
Wajumbe wa Mtandao wa Wabunge wa kupambana na Rushwa wakiwa katika semina ya mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa sheria ya wakala wa vipimo na mizani iliyofanyika leo tarehe 26 Januari, 2019 katika hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma.PICHA NA OFISI YA BUNGE)


Na.Alex Sonna,Dodoma

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano La Tanzania Job Ndugai amesema bado kuna tatizo kubwa katika vipimo sahihi wakati wa ununuzi wa mazao kutoka kwa wakulima licha ya kuwepo kwa Sheria ya vipimo.

Hayo ameyasema leo jijini Dodoma alipokuwa akifungua Semina ya wabunge juu ya changamoto na mafanikio ya sheria ya vipimo ikiwa ni pamoja na wabunge hao kutoa michango yao katika semina hiyo jinsi ya kupambana na rushwa katika vipimo.

Wabunge hao ni wanachama wa hiari wa chama cha kupambana na vitendo vya rushwa APNAC ambao hutoa michango juu ya kupambana na rushwa na kuifikisha panapo husika.Spika amesema kuwa wakulima wamekuwa wakinyonywa sana na baadhi ya wafanyabisha kwa kutumia vipimo ambavyo si sahihi ikiwemo ufungaji wa mazao kwa njia ya lumbesa.

“Rasilimali nyingi zimekuwa zikipotea kutokana na ufungashaji kwa njia ya lumbesa , na nyinginezo ambazo si rasmi tufikie wakati tuwe na sheria kali zaidi kwani wakulima wetu wamenyonywa na kupunjwa vya kutosha” amesema Ndugai

Akitolea ufafanuzi kuhusiana na vipimo vya magari ya mizigo Spika alishangazwa kuona kuwa magari hayo licha ya kupita katika mizani mbalimbali lakini bado yanzuiwa sehemu Fulani kwa sababu ya kutakiwa kupimwa tena.

Aidha amesema kuwa hali hiyo imekuwa ikiwakera wananchi kwani hawaelewi nini tatizo mpaka kuwepo kwa vipimo kila sehemu na kufanya msururu wa magari kuwa mkubwa kusubiri kupimwa.“Kama ni magari ya mizigo inawezekana wakaongeza njiani lakini kama wale wanaosafirisha mafuta kweli jamani tuliangalie na hilo tuliangalie” amesisitiza

Spika Ndugai amesema kuwa hali hiyo ni chimbuko la rushwa kwani kama mfanyabishara anayesafirisha mafuta ameshapima vituo vyote hakuna sababu ya kumzuiakwani uwezekano wa kuongeza ujazo wa mafuta njiani ni mdogo.

Awali akitoa taarifa ya awali kwa wabunge wanachama wa chama cha wabunge wanapambana na rushwa (APNAC) Katibu wa APNAC Daniel Mtuka alisema APNEC iliundwa mwaka 2000.Hata hivyo amesema kuwa madhumuni ya kuundwa kwake ni kupambana na rushwa mara baada ya kuona vitendo vya rushwa vinazidi.

Pia amesema kuwa wabunge waliokuwepo kipindi hicho waliona kuna umuhimu wa kuanzisha kikundi cha wabunge ambao watapambana na rushwa.Spika Ndugai amesema kuwa APNAC ilifanikiwa mwaka 2007 kushiriki kuandaa sheria namba 11 ya TAKUKURU ambapo sheria hiyo ilikuwa na vifungu vine tu lakini sasa vipo 24

Amesema kuwa bado Sheria ya Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa inahitaji marekebisho zaidi. Alisema kutokana na hali hiyo APNAC ilita mawazo wakati wa mchakato wa Bunge la katiba ambao alisema ungewabana zaidi wanaokamatwa na vitendo vya rushwa.

“Tumeweza kutoa marekebisho mengi juu ya Sheria ya TAKUKURU na mengi yameweza kusaidia nchi yetu lakini bado tunaona ipo haja ya kuendelea kutoa mawazo yetu.Kwa upande wa vipimo Waziri wa Biashara na Viwanda Josph Kakunda amesema kuwa bado kuna changamoto kubwa katika suala la vipimo.Hata hivyo amesema kuwa kumekuwa na udanganyifu mkubwa kwa wafanyabiashara na madalali wanunuapo amzao toka kwa wakulima .

“Vipimo kama vya Lumbesa, Madebe na hata vikopo bado vimekuwa vikitumika katika sehemu nyingi hapa nchini ingawa tunavikataa” amesema
Amesema kuwa Wizara yake imeweza kujenga vituo vya msoko katika mipaka ili wakulima waweze kuuza mazao yao kihalali na uzito unaotakiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...