WAKALA
wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA), imewajengea uwezo na kuwapa mbinu
za kutafuta ajira pindi wanapomaliza masomo zaidi ya wanafunzi 500 wa
Chuo cha Ufundi Arusha (ATC).
Huduma zinazotolewa na TaESA ni kuunganisha watafuta kazi na waajiri, kutoa mafunzo kuhusu mbinu za usaili ambayo huwajengea uwezo wa kujiamini, kutoa ushauri kuhusu masuala ya ajira na kutoa taarifa za soko la ajira.
Akizungumza mjini Arusha Afisa Kazi Mwandamizi wa TaESA na Mratibu wa Mafunzo hayo kwa wanafunzi Peter Ugata alisema, Tanzania na dunia kwa sasa kuna changamoto zinazohusiana na Soko la Ajira. Alisema hatua hiyo imechangiwa na mahitaji ya Waajiri kuhamia kwa watu wenye ujuzi wa ziada mbali ya na weledi wa kusomea, kwani mara nyingi ujuzi wa ziada hausomewi.
“Changamoto zilizopo zimeletwa na mabadiliko ya dunia ya utanfawazi ambapo watu, huduma na bidhaa ziko huru kutoka sehemu moja hadi nyingine. “Ili kukabiliana na hali hiyo nchi mbalimbali duniani zilianzisha huduma za Ajira kupitia Sera, Sheria, Kanuni na maazimio ya Shirika la Kazi Duniani (ILO),” alisema.
Akifafanua namna huduma za ajira zinavyotolewa Ugata alisema Wakala husajili na kutunza taarifa za watafuta kazi kwa kutumia Kanzidata iliyopo. “Wakala huoanisha sifa za mtafuta kazi kulingana na mahitaji ya kazi husika kama yalivyoanishiwa na mwajiri, lakini pia wakala unaoanisha ujuzi, uzoefu, elimu na sifa nyingine za watafuta kazi na mahitaji ya sifa za kazi za mwajiri,” alisema Ugata.
Anazitaja baadhi ya faida za kutumia TaESA ni Waajiri kupewa ushauri mzuri kuhusu mwenendo wa soko la Ajira na mahitaji na aina ya watu na ujuzi utaokamsaidia kuleta tija. “TaESA itamuwezesha mwajiri kupata wafanyakazi kazi waadilifu na waaminifu katika kazi, wabunifu na wakujituma kazini , lakini pia kuiwezesha serikali kupata takwimu za uamuzi na mipango kwa haraka,” alisema Ugata.
TaESA inafanya kazi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu.
Huduma zinazotolewa na TaESA ni kuunganisha watafuta kazi na waajiri, kutoa mafunzo kuhusu mbinu za usaili ambayo huwajengea uwezo wa kujiamini, kutoa ushauri kuhusu masuala ya ajira na kutoa taarifa za soko la ajira.
Akizungumza mjini Arusha Afisa Kazi Mwandamizi wa TaESA na Mratibu wa Mafunzo hayo kwa wanafunzi Peter Ugata alisema, Tanzania na dunia kwa sasa kuna changamoto zinazohusiana na Soko la Ajira. Alisema hatua hiyo imechangiwa na mahitaji ya Waajiri kuhamia kwa watu wenye ujuzi wa ziada mbali ya na weledi wa kusomea, kwani mara nyingi ujuzi wa ziada hausomewi.
“Changamoto zilizopo zimeletwa na mabadiliko ya dunia ya utanfawazi ambapo watu, huduma na bidhaa ziko huru kutoka sehemu moja hadi nyingine. “Ili kukabiliana na hali hiyo nchi mbalimbali duniani zilianzisha huduma za Ajira kupitia Sera, Sheria, Kanuni na maazimio ya Shirika la Kazi Duniani (ILO),” alisema.
Akifafanua namna huduma za ajira zinavyotolewa Ugata alisema Wakala husajili na kutunza taarifa za watafuta kazi kwa kutumia Kanzidata iliyopo. “Wakala huoanisha sifa za mtafuta kazi kulingana na mahitaji ya kazi husika kama yalivyoanishiwa na mwajiri, lakini pia wakala unaoanisha ujuzi, uzoefu, elimu na sifa nyingine za watafuta kazi na mahitaji ya sifa za kazi za mwajiri,” alisema Ugata.
Anazitaja baadhi ya faida za kutumia TaESA ni Waajiri kupewa ushauri mzuri kuhusu mwenendo wa soko la Ajira na mahitaji na aina ya watu na ujuzi utaokamsaidia kuleta tija. “TaESA itamuwezesha mwajiri kupata wafanyakazi kazi waadilifu na waaminifu katika kazi, wabunifu na wakujituma kazini , lakini pia kuiwezesha serikali kupata takwimu za uamuzi na mipango kwa haraka,” alisema Ugata.
TaESA inafanya kazi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu.
Afisa
Kazi kutoka TaESA Emma Mangesho akiwajengea uwezo na kuwapa mbinu
Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), kuhusu namna bora ya kutafuta
kazi
Meneja
wa Karakana ya uchomeleaji Chuo cha Ufundi Arusha Expedito Miliaso
akiwaonyesha maofisa wa Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA),
vifaa vipya vya uchomeleaji wanavyotumia wanafunzi wa Chuo hicho kwa
ajili ya mafunzo.
Maofisa
wa Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA) kutoka Dar es Salaam na
Arusha wakiangalia kifaa maalumu cha uchomeleaji ndani ya Karakana ya
Chuo cha Ufundi Arusha anayewaonyesha ni Meneja wa Karakana ya
uchomeleaji Expedito Miliaso.
Baadhi
ya Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakimsikiliza Afisa Kazi
wa Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESO) kutoka Dar es Salaam Emma
Mangesho akifundisha namba bora ya uandishi wa barua za kuomba ajira.
Afisa
Kazi wa Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESO) kutoka Dar es Salaam
Emma Mangesho akifundisha wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC),
mbinu za kuomba ajira ikiwamo namna bora ya uandishi wa barua za kuomba
kazi.
Afisa
Kazi Mwandamizi kutoka Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA) na
Mratibu wa mafunzi Peter Ugata akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha
Ufundi Arusha (ATC) wakati wa kuwajengea uwezo wa namna bora ya kutafuta
kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...