Baba mzazi wa wasanii wa bongofleva nchini Ali kiba pamoja na Abdul kiba Mzee salehe Kiba amefariki leo alfajiri katika hospital ya Taifa Muhimbili alipokua akipatiwa matibabu.
Taarifa za awali zianeleza kuwa msiba huo utakuwa karikaoo nyumbani kwa marehemu Mzee salehe kiba.
Taratibu za Mazishi bado zinaendelea kupangwa na wanafamilia ili kuupumzisha mwili wa Mzee kiba mahali pema.
Uongozi wa Michuzi Media Group unatoa pole kwa familia ya Mzee kiba na kwa wale wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki kigumu.
TUTAWALEZA TAARIFA ZAIDI KUHUSIANA NA MSIBA HUU.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMIN
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...