Na Agness Francis, Blogu ya Jamii. 

KATIKA mchakato  wa kuendelea kwa michuano ya Kombe la Shirikisho (ASFC)  Uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)  imetangaza kuwa itafanya droo ya Kombe hilo siku ya kesho Januari 10 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa Hababari katika ofisi za TFF jijini Dr es Salaam. Afisa habari wa TFF Cliford Ndimbo amesema, droo hiyo itakafanyika katika Makao Makuu ya Azam Tv, iliyopo Tabata majira ya saa 5 asubuhi na itahusisha raundi ya 4 zenye timu 32 na raundi ya 5 itakayohusisha timu 16.

Ndimbo amesema timu zilizobaki katika hatua hiyo ni  Young Africans SC, Azam FC, Lipuli FC, Mtibwa Sugar, KMC, Coastal Union, Kagera Sugar, Mbeya City, Stand United, JKT Tanzania.

Nyingine ni Singida United, Alliance FC, African Lyon, Biashara United, Boma, Namungo, Mbeya Kwanza, Friends Rangers, Majimaji FC, Dodoma FC, Pamba SC, Rhino Rangers, Reha FC, Dar City, Polisi Tanzania, Mashujaa, Transit Camp, The Mighty Elephant, Cosmopolitan, Kitayosce, La Familia FC, Pan African

Ameongeza, mshindi atakaeibuka katika mashindano  hayo ataipeperusha bendera na  kuwakilisha nchi katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika, ambapo mwaka jana Mtibwa Sugar ndio waliibuka kidedea wa michuano hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...