Na Ripota Wetu

UMOJA wa Afrika umetoa mwito wa kuaihirisha kwa muda wa kutangaza matokeo rasmi ya uchaguzi wa Rais unaozusha mabishano katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kwa sababu ya "shaka shaka kubwa ."

Imeelezwa kuwa Wawakilishi wa Umoja wa Afrika wamekutana leo Januari 18,2019 Mjini Addis Ababa na kisha wakakubaliana kutuma ujumbe wa ngazi ya juu mjini Kinshasa kwa lengo la kusaka njia za kuupatia ufumbuzi mzozo 
wa kisiasa.

Viongozi wa Taifa na Serikali wanaohudhuria mkutano huo wamekiri kuwa kuna mashaka makubwa hasa kuhusu ulinganifu wa matokeo ya awali kama yalivyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi (CENI) na yale ya kura zilizopigwa.

Umoja wa Afrika umesema katika taarifa yake. "Ingawa hali ni tulivu hadi sasa, lakini wasi wasi umetanda pia, amesema mwenyejkiti wa Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat mbele ya viongozi wakiwemo pia wale wa Afrika 

Kusini, Zambia, na Jamhuri ya Congo waliokutana kuzungumzia matokeo yanayobishwa ya uchaguzi katika jamhuri ya kidemokrasi ya Congo. Serikali mjini Kinshasa imeukosoa wito wa Umoja wa Afrika na kusema korti ya nchi hiyo ni huru. Korti ya Katiba inasikiliza malalamiko ya Martin Fayulu dhidi ya matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais.

CHANZO -DW 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...