NA K-VIS BLOG/Khalfan SaidMITAMBO ya kufua umeme wa gesi asilia kwenye kituo cha Kinyerezi II jijini Dar es Salaam imetumia teknolojia ya kisasa kabisa ijulikanayom kama combine cycle na kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki kutumia teknolojia hiyo. 

Akifafanua kuhusu teknolojia hiyo, Meneja Miradi (uzalishaji) wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO, Mhandisi Stephene S. A. Manda, amesema baada ya mitambo ya kufua umeme utokanao na gesi, mvuke unaozalishwa kwa awamu ya kwanza kutokana na joto hupelekwa tena kwenye mtambo mwingine na huko unazalisha umeme wa awamu ya pili. 

Alisema, tayari TANESCO imepokea maombi kutoka nchi mbalimbali zikiwemo zile za SADC kuja kujifunza teknolojia hiyo, ambapo katika mitambo nane ya kufua umeme iliyoko Kinyerezi II, miwili ni ile itokanayo na mvuke (steam turbines) “Tulivyokuwa na mkutano wa SAPP kule Arusha yaani Southern Africa Power Pool nchi mbalimbali zimeonyesha nia ya kuja kujifunza teknolojia hii.” Alisema. Mhandisi Manda ametoa wito kwa vyuo mbalimbali vinavyotoa taaluma ya uhandisi wa umeme kupeleka wanafunzi ili wajifunze teknolojia hiyo ya kisasa. “Wanafunzi wanao….Practice engineering wako kwenye field ambao hawajaona teknolojia inavyofanya kazi waje wajifunze.” Alisema.

Moja ya mitambo ya kufua umeme utokanao na mvuke (steam turbine) kwenye kituo cha kufua umeme wa gesi asilia Kinyerezi II jijini Dar es Salaam.

Meneja Miradi (uzalishaji) wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO, Mhandisi Stephene S. A. (kulia) na Meneja wa kituo cha kufua umeme wa gesi cha Kinyerezi II, Mhandisi Ambakisye Mbangula, (katikati), wakimsikiliza mhandisi huyu kutoka nje anayehudumu kwenye mitambo hiyo wakati huu wa kumalizia ujenzi.

Mhandisi Manda akifafanua kuhusu mitambo ya kisasa iliyofungwa kwenye kituo hicho.

Mhandisi Manda akizungumza na wafanyakazi wa TANESCO kwenye chumba cha udhibiti mwenendo wa mitambo ya umeme (control room) Kinyerezi II.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...