WAZIRI wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani, Heiko Maas yuko ziarani mjini Moscow kwa mazungumzo pamoja na
Waziri mwenzake Sergei Lawrov kuhusu mzozo wa Ukraine na vita nchini Syria.
Kwa mujibu wa DW ni kwamba mvutano kati ya Urusi na Ukraine umezidi makali mnamo siku za hivi karibuni baada
ya korti moja ya mjini Moscow kurefusha hadi kati kati ya mwezi wa April unaokuja, muda wa kushikiliwa kizuwizini
wanamaji 24 wa Ukraine waliokamatwa mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka jana .
Baada ya mazungumzo yake mjini Moscow, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ujerumani Heiko Maas amepangiwa
kwenda Kiew baadae leo kwa mazungumzo pamoja na waziri mwenzake Pawel Klimkin.
CHANZO-DW
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...