MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji sehemu ya matofali aliyotoa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ili wanafunzi wapata fursa ya kusoma
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akilakiwa na wanafunzi wa shule ya Sekondari Pongwe Jijini Tanga wakati alipokwenda kuwakabidhi matofali na mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akikagua madarasa kwenye ambayo hayajakwisha kwenye shule ya Sekondari Pongwe kabla ya kuwakabidhi mifuko ya saruji na matofali  kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na kushoto ni Diwani wa Kata ya Pongwe(CCM) Mbaraka Sadi
Diwani wa Kata ya Pongwe(CCM) Mbaraka Sadi akizungumza kulia ni MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi mifuko ya saruji Diwani wa Kata ya Pongwe (CCM) Mbaraka Sadi kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasaa kwenye kata yake
sehemu ya mifuko ya saruji ilioyotolewa na Waziri Ummy
 Sehemu ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Pongwe wakifuatilia hotuba ya MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katika akiwa kwenye picha ya pamoja na walimu wa shule ya Sekondari Pongwe
 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoani Tanga(CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwa katikati ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Mikanjuni mara baada ya kukabidhi msaada wa matofali na mifuko ya saruji
 Sehemu ya wananchi wakifuatilia matukio kwenye hafla hiyo

 


Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Tanga na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu leo amekabidhi matofali 3,500 zenye thamani ya shilingi milioni 5.6 na mifuko ya Saruji 250 yenye thamani ya shilingi milioni 3 ili kuweza kusaidia kutatua tatizo la uhaba wa madarasa.

Msaada huo aliuta  kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa ya Sekondari zilizopo katika Jiji la Tanga ambazo ni Shule za Sekondari   Pongwe, Maweni, Mikanjuni, Horten na Kiomoni ambapo kila shule imepatiwa Matofali 700 na saruji mifuko 50.

Akizungumza ktk makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Shule ya Sekondari Mikanjuni, Waziri Ummy ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoani Tanga (CCM)alieleza kufurahishwa na jitihada za Mhe Rais Dr. John Pombe Magufuli za kuboresha Elimu nchini na katika Jiji la Tanga

Alisema juhudi hizo zimesaidia  kuwezesha uwepo wa idadi kubwa ya wanafunzi waliofaulu kujiunga na Elimu  ya Sekondari katika Jiji la Tanga. Hivyo yeye kama mbunge ameona anao wajibu wa kuchangia ujenzi wa madarasa ili kuwezesha watoto wote 6,024 wa Jijini Tanga waliofaulu Elimu ya Msingi kuendelea na Elimu ya Sekondari.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tanga  Tobias Mwilapwa alisema katika mwaka huu 2019 jumla ya wanafunzi 6,024 wamefaulu kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza katika Jiji la Tanga kutoka wanafunzi 5,332 mwaka 2018.
Hali hii imesababisha mahitaji zaidi ya Vyumba vya madarasa 71 ili kumudu kuchukua ongezeko la wanafunzi 1,324 waliofaulu kwenda Sekondari katika Jiji la Tanga.

Makabidhiano hayo yamehudhuriwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Tanga Ndugu Kidima, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga, Bwana Daudi Mayeji, Waheshimiwa Madiwani wa Kata husika, Watendaji wa Idara ya Elimu na Bodi za Shule husika.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...