Na Ahmed Mahmoud Arusha
Serikali za Canada na Tanzania zinaendesha mradi wa miaka mitano wenye lengo la kusaidia vijana kuweza kuwa na umahiri wa kujiajiri na kujifunza kwa kutenda.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa vyuo vya ufundi nchini Dkt.Noel Mbonde wakati akifungua semina ya mradi huo inayoendelea jiji Arusha na kubainisha kuwa mradi huo utafikia malengo ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa Kati wa viwanda.

Amesema kuwa mradi huo ulionza mwaka 2014 unatarajiwa kufika tamati Machi mwakani utasaidia Sana vijana kwani unalenga kumuwezesha kijana na mwalimu kuwa karibu na umeleta mabadiliko chanya nchini.

"Serikali imejipanga kuhakikisha mradi huu unakuwa endelevu baada ya kumalizika kwani tuna miradi mingi inaendeshwa nchini yenye lengo la kuongeza weledi kwa vijana wetu kuweza kufikia adhma ya serikali ya uchumi wa Kati wa viwanda"alisema Dkt.Mbonde.

Kwa upande wake mwakilishi wa Balozi wa Kanada nchini Tanzania bi Nathalie Garon amesema kuwa serikali ya nchi yake itaendeleza ushirikiano wa dhati kuhakikisha vijana wa kitanzania wanafikia malengo endelevu na nchi inapiga hatua.

Amesema MAFUNZO hayo ni moja ya ushirikiano Kati ya nchi yake na serikali ya Tanzania kuonyesha jinsi wanavyothamini vijana katika suala zima la KUKUZA maendeleo ya bara la Afrika.
Mwakilishi wa balozi wa Canada nchini bi Nathalie Garon ambaye pia ni karibu wa Kwanza wa maendeleo na kiongozi wa ukiaji endelevu wa uchumi wa ubalozi huo akifungua semina ya mradi wa kusaidia vyuo vya ufundi nchini unaondelea. Kwenye chuo cha Veta njiro jijini Arusha picha na Ahmed Mahmoud Arusha.
Mkurugenzi wa elimu ya ufundi wizara ya elimu na ufundi Dkt.Noel Mbonde akizungumza kwenye semina ya mradi wa kusaidia vyuo vya ufundi nchini iliyofanyika kwenye chuo cha Veta Njiro jijini Arusha picha na Ahmed Mahmoud Arusha 

Tom Tunney meneja mradi wa ushirikiano na serikali za Canada na Tanzania kuhusu mafunzo ya kukuza maarifa kwenye sekta ya ajira rasmi na isiyo rasmi akitoa mada kwenye semina ya mafunzo yaliowakutanisha wakuu wa vyuo vya ufundi (veta) inayofanyika jijini Arusha picha na Ahmed Mahmoud Arusha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...