Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la  kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2001
Baadhi ya watumishi wa umma wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha  wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani), wakati wa kikao kazi cha watumishi hao na Naibu Waziri huyo chenye  lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla ya kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2003
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Bi. Theresia Mbando akitoa neno la utangulizi kumkaribisha Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Mji Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao  chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao, kabla kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF katika Halmashauri hizo mkoani Pwani.
IMG_2004
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akitoa onyo kwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Bi. Ruth Mwelo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu  wa Halmashauri hiyo kwa kumtolea lugha chafu mstaafu aliyekuwa akidai haki yake, onyo hilo amelitoa wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi hao.

……………………
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) amempa onyo kali Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Bi. Ruth Mwelo ambaye ni Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu  wa Halmashauri hiyo kwa kumtolea lugha chafu mstaafu aliyekuwa akidai haki yake na kumtaka afisa huyo ajirekebishe haraka iwezekanavyo.

Onyo hilo amelitoa wilayani Kibaha, wakati wa kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji, kabla ya kutembelea wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika wilaya hizo ili kujiridhisha na utekelezaji wake.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema, haiwezekani afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu za kiutumishi ndio awe kikwazo cha utendaji kazi katika Halmashauri hiyo kwa kutoa lugha chafu dhidi ya wanaofuta huduma ofisini kwake, na kuongeza kuwa, afisa huyo ndiye anayestahili kuwa kwenye Kamati ya Maadili ili kutoa miongozo ya uadilifu na kusimamia maadili ya watumishi kwa ujumla katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

Mhe. Dkt. Mwanjelwa amemtaka afisa huyo kutotumia cheo chake vibaya na badala yake asimamie vema nidhamu na masilahi ya watumishi wa umma.
Sanjari na hilo, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amemtaka afisa huyo kuacha tabia ya kutoa siri za ofisi na kutokuwa mchonganishi miongoni mwa watumishi wenzie kwani matendo hayo hayapaswi kufanywa na mtumishi yeyote nchini.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwanjelwa amesema ameamua kuweka bayana  mapungufu ya afisa huyo mbele ya watumishi wenzie ili ajifunze kutokana na matendo yake yasiyoridhisha na aweze kubadili mwenendo wake mbaya wa kimaadili.
Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) ameendelea kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma nchini, kwa kutoa onyo kwa watumishi wote wanaobainika  kukiuka Kanuni za Maadili ya Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...